Thursday, October 3, 2013

Profesa Jay Ampigia Salute JCB


NYOTA wa Hip Hop  nchini Joseph Haule maarufu kama Professa Jay amesema ujumbe ulioko kwenye wimbo wa msanii wa Arusha Jacob Makala maarufu kama JCB umemgusa, hivyo kuamua kushirikiana naye katika kuelimisha jamii.
Akizungumza na gazeti hili, Professa Jay alisema wimbo huo unaofahamika kama ‘Drive Slow” unahamasisha madereva wote nchini kuendesha vyombo vya usafiri taratibu ili kuokoa maisha ya watu wanaogongwa na kufa na wengine wakibaki na ulemavu wa maisha.
“Madereva wengi wamekuwa wakiendesha magari au pikipiki kwa kasi bila kuangalia watu wengine wanaotembea kwa miguu, kiasi kwamba huwagonga na kusababisha vifo, hivyo nimeamua  kushirikiana na JCB katika kuhamasisha jamii kubadilika ili kuokoa maelfu ya watu,”alisema.
Professa Jay ambaye alimpoteza mama yake mzazi kwa ajali, alisema aliguswa na ujumbe huo na anaamini wengi wakiusikia watajifunza na kubadilika mara moja.
Licha ya wimbo huo kumgusa, alisema JCB ni msanii anayemkubali na amekuwa na ndoto ya kufanya kazi pamoja kwa muda mrefu ndio maana wameamua kushirikiana kutimiza malengo ya msanii huyo.

0 comments:

Post a Comment