
MSANII wa kizazi kipya Erick Msodoki maarufu kama ‘Young Killer’ amewaonya baadhi ya watu ambao humpigia simu na kumsumbua bila sababu za msingi, kuacha tabia kwa vile humkera.
Msodoki
alisema anashangazwa na baadhi ya watu hasa wanawake wamekuwa wakimpigia simu,
wengine wakimtaka kimapenzi kitendo ambacho hakimfurahishi na ni kero.
“Siku hizi kuna baadhi ya wanawake wananipigia
simu wakinitaka, naomba waache tabia hiyo, sipendi usumbufu, kwani mimi bado
mdogo, naomba mniache,”alisema.
Msanii
huyo ambaye kwa sasa anavuma na ‘Mrs Superstar’ alisema anashangazwa watu hao
wamepata wapi namba yake, kwasababu hakuigawa hadharani kwa kukwepa usumbufu wa
aina hiyo.
Alisema
ni bora kama wangekuwa wanapiga simu kumuunga mkono kwenye kazi zake, kuliko
kumpigia simu na kumweleza mambo ambayo hayaendani na umri wake.
0 comments:
Post a Comment