Thursday, October 3, 2013

Polisi wamtoa Kelly Khumalo tamashani

MWANAMUZIKI mtata katika tasnia ya muziki Afrika Kusini, Kelly Khumalo, amepata aibu ya mwaka baada ya polisi kumtoa katika tamasha mjini Soweto na kumhoji kwa shambulio.
Khumalo alikuwa anasakwa na Polisi wa Kituo cha Hillbrow, mjini hapa baada ya kudaiwa kumshambulia mke wa golikipa wa timu za Orlando Pirates na Bafana Bafana, Senzo Meyiwa kutokana na masuala yanayohusishwa na mapenzi.
Ofisa mmoja polisi anayefahamu kesi hiyo alisema ofisa upelelezi na mwenzake mmoja walienda nyumbani kwa wazazi wa Khumalo, Vosloorus Jumamosi iliyopita mchana lakini hawakumkuta.
Mtoa taarifa wao aliwaeleza kuwa Khumalo anatarajia kutoa burudani jioni hiyo katika ukumbi wa Jabulani Amphitheatre mjini Soweto. Ndipo maofisa hao walipoenda eneo hilo lililokuwa limejaa watu na kumkuta akijiandaa kupanda jukwaani na bendi yake.
Maofisa hao walimwamuru kutoke nje akiwa mbele ya umati wa mashabiki, na walimtaka awafuate katika gari lao la polisi ambapo walichukua maelezo yake na kuondoka.
 “Polisi watapeleka maelezo ya mwanamuzidiki huyo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka ili afanye maamuzi kama ashtakiwe au la. Lakini kwanza watatakiwa kuchukua maelezo ya dada yake Kelly na  Senzo. Kinachowachanganya wapelelezi ni kitendo cha Senzo kutotoa ushirikiano jambo ambalo linafanya Mandisa akose haki yake haraka,” alisema mtoa habari.
Kwa mujibu wa maelezo yaliyoko polisi, Khumalo alimkuta Meyiwa akizungumza na mkewe, Mandisa, barabarani. Ndipo mwanamuziki huyo alipoegesha gari lake na kuwafuata. 
Inadaiwa Mandisa alienda upande wa abiria na alijaribu kufungua mlango lakini ukawa umefungwa. Kisha alirudi kwa Meyiwa na kumtaka afungue mlango, lakini ghafla inadaiwa sasa mdogo wa Khumalo aliyekuwa amekaa katika gari la msanii huyo alishuka na kuanza kumshambulia Mandisa.
“Mandisa alipata majeraha usoni baada ya Khumalo ma mdogo wake kumkwaruza kwa makucha yao usoni,” alisema ofisa huyo.

0 comments:

Post a Comment