MWANAMUZIKI Katy Perry amekiri kuwa alipata mawazo
ya kujiua baada ya kutengana na mumewe mchekeshaji, Russell Brand.
Perry ambaye alitengana na mchekeshaji huyo wa
Uingereza Desemba 2011 baada ya ndoa yao kudumu kwa miezi 14, alikiri kuwa
alikuwa mkiwa na akajikuta akipata maswali kichwani iwapo aendelee kuishi au la.
Mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 28, ambaye
sasa ana uhusiano na John Mayer, anazungumzia kutengana na mumewe katika wimbo Ghost
na By The Grace of God ambazo ziko
katika lalbamu yake ijayo ya Prism.
Perry alilieleza Jarida la Billboard kuwa, "
wimbo huo ni ushahidi jinsi gani hali ilivyokuwa ngumu wakati fulani. Nilijiuliza,
'je nataka kuvumilia? Je, niendelee kuishi?
Mwanamuziki huyo ambaye albamu yake mpya
inatarajiwa kuzinduliwa Oktoba 18, hivi karibuni aliuza jumba lake la kifahari
lenye thamani ya Dola za Marekani milioni 6.5 West Hollywood, California, nyumba
ambayo alikuwa akiishi na mumewe Russell.
0 comments:
Post a Comment