
MWANAMITINDO Flaviana Matata ameyataka
makampuni,mashirika pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo ya elimu kuwasaidia
wanafunzi wenye uhitaji maalumu.
Flaviana hivi majuzi alitoa misaaa ya madaftari
800 pamoja na kalamu 800 kwa wanafunzi wa shule ya msingi Minazini iliyopo
Mwananyamala.
Flaviana aliyasema hayo wakati akizungumzia
harakati zake za kuchangia elimu kwa kuwanunulia vifaa vya shule wanafunzi
wenye uhitaji maalum.
Alisema kuwa wapo wanafunzi ambao wanashida hasa
katika suala zima la kupata vifaa vya shule kama vile kalamu, madaftari, mabegi
na huduma nyingine muhimu.
Alisema kuwa ili kukabiliana na changamoto ni
vema makampuni yakajitokeza kuungana mkono na harakati zake katika kuwahudumia
wanafunzi.
"Kupitia Taasisi yangu ya Flaviana Matata
Foundation kwa sasa tunajihusisha na utoaji wa vifaa vya shule ili kuwasaidia
wanafunzi wenye uhitaji maalum hapa nikiwa namaanisha kuwa wanafunzi ambao
wazazi wao hawana fedha za kuwanunulia vifaa vvya shule au hata wale ambao ni
yatima wanatakiwa kulelewa"alisema Flaviana.
Flaviana aliyakaribisha makampuni kuwanunulia
wanafunzi hao vifaa vya shule kupitia Taasisi yake hiyo na kuongeza kuwa kwa
kufanya hivyo wanakuwa wamechangia pia fedha za kusaidia harakati nyingine za
kijamii.
Aliongeza kuwa vifaa vya shule vina nembo ya
jina la Taasisi yake na kwa kampuni itakayonunua bidhaa za kusaidia wanafunzi
kupitia kwake itatajwa pia katika vifaa hivyo.








0 comments:
Post a Comment