Mkurugenzi
Mtendaji wa kampuni ya Simba Logistic and Equipment Fareed Nahdi akirusha kifaa
cha Bonex katika moto kwa ajili ya kuzima moto uliowashwa wakati wa uzinduzi wa
kifaa hicho.
Mtoto
akionesha namna ya kutumia kifaa hicho kuzimia moto.

Kamishna
wa kikosi cha zimamoto Rogatius Kipali akizima moto katika kuonesha ubora wa
kifaa hicho.

Meneja
Mradi wa teknolojia ya Bonex Lura Lyabandi akiwafafanulia wageni.
TEKNOLOJIA ya aina mbalimbali zinazidi kukua na
kusaidia kwa kiasi kikubwa kutatua kero mbalimbali hapa nchini.
Katika jiji la Dar es salaam kama majiji mengine
nchini kero kubwa mojawapo ni upatikanaji wa utatuzi wa haraka wa kukabiliana
na janga la moto.
Kutokana na miundombinu mibovu ya barabara ya
jiji hili kikosi cha zima moto kimekuwa kikikumbana na kero kubwa ya kufika
haraka katika maeneo mbalimbali ambapo moto unawaka.
Mbali na barabara kuwa ni kikwazo kikubwa lakini
pia kerokubwa ni mkusanyiko wa nyumba nyingi katika eneo moja yaani unakuta
kuna maeneo ambapo gari haliwezi kufika kutokana na mkusanyiko wa nyumba.
Hali hiyo inapelekea nyumba nyingi kuungua moto
na kupelekea upotevu wa mali nyingi za watu kwa kuwa moto ukizuka kwenye nyumba
moja na kushindwa kuzuiliwa mapema basi unaunguza na nyumba za jirani.
Katika kukabiliana na hali hiyo kumekuwa na
mikakati mbalimbali ambayo Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi kupitia kikosi cha
usalama barabarani imekuwa ikiendesha mafunzo ya aina mbalimbali ya kuzuia
moto.
Mafunzo hayo yamesaidia kikosi hicho katika
kukabiliana na majanga mbalimbali ya moto lakini hata hivyo imekuwa ni shida
katika maeneo yasiyofikika kiurahisi na haraka.
Katika kukabiliana na janga kampuni ya Simba
Logistic Equipment Co Ltd imezindua kifaa kipya kiitwacho Bonex ambacho
kinabebeka kirahisi.
Kifaa hicho inaonekana kuwa ni teknolojia mpya ambayo inalenga kusaidia
kutatua kero ya muda mrefu ya kutabiliana na janga la moto.
Kifaa ni cha kurusha ambapo iwapo moto umezuka
ghafla sehemu kinachotakiwa kufanyika ni kuchukua kifaa hicho na kisha kukitupa
katike eneo ambalo moto umewaka.
Bonex ni chupa ambayo ni ya plastic ambayo ndani
yake ina kimiminika chenye kemikali hiyo ya kuzima moto kwa kiwango kikubwa.
Mkurugenzi wa kampuni hiyo Fareed Nahdi anasema
kuwa kifaa hicho kinalenga kusaidia utoaji wa huduma ya uzimaji moto kwa
urahisi zaidi.
Anasema kuwa ni rahidi kutumia kwa kuwa ni kifaa
cha kurusha tu katika moto na kisha kinazima moto.
"Najua ukilinganisha na teknolojia nyingine
inavyofanya kazi hii ni tofauti kwa kuwa vifaa vingine unatakiwa kufuata
taratibu ambazo ni ndefu kidogo kwanza ujue namna ya kuvifungua na kisha ndio
kuelekeza kwenye moto tena kwa kuwa
umesogelea" alisema Nahdi.
Alisema kuwa pia inatakiwa kufanyiwa kwanza
mafunzo ya kuelekezwa namna ya kutumia lakini hiki unarusha tu kwenye moto na
kinazima kwa kiasi kikubwa.
Kwa upande wake Kamishna wa kikosi cha Zimamoto
Tanzania, Rogatius Kipali anasema kuwa ofisi yake inatambua juhudi zinazofanywa
na wadau wengine mbalimbali katika kukabiliana na janga la moto.
Anasema kwa mfano mzuri ni kifaa hicho ambacho hata mama wa nyumbani
anaweza kukitumia kuzimia moto iwapo imetokea katika mazingira ya nyumba yake.
" Najua ndio kuzima moto ni kazi yetu
lakini ikumbukwe kuwa pale unapotokea kunatakiwa kuwe na hatua za awali za
kufuatwa katika kuuzima na ndio hivyo hivyo ambavyo hawa watu wa Simba Logistic
wamekuja na kifaa hichi muhimu"anasema Kipali.
Kwa upande wake Kamanda wa Kikosi cha Usalama
barabarani Mohamed Mpinga anasema kuwa kifaa hicho kinaweza kusaidia kuzuia
ajali za moto katika magari kwa kuwa ni rahisi kutumia.
Kwa upande wetu kikosi cha usalama barabarani
tunaona kuwa kifaa hiki pia ni mkombozi kwa kuwa kwanza hakihitaji ukarabati
kama vifaa vingine vya kuzimia moto"anasema Mpinga.








0 comments:
Post a Comment