Monday, November 25, 2013

Nguvu za Zitto, Udhaifu wa Mbowe Moja ya Chanzo cha Mgogoro CHADEMA



KATIKA moja ya mambo yaliyojitokeza katika mgogoro wa uongozi wa Chadema, ni tathmini ya nguvu za aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu, Kabwe Zitto dhidi ya kinachoitwa udhaifu wa Mwenyekiti wa sasa wa chama hicho, Freeman Mbowe na uongozi wake.
Tathmini hiyo ambayo aliyekuwa mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Dk Kitila Mkumbo jana ameiita kuwa ni siri iliyowekwa wazi kwa makosa ya kijinga, imeeleza namna kiongozi huyo alivyoandaa mkakati wa kumuondoa Mbowe madarakani kidemokrasia, kupitia nguvu za Zitto.
“Nani tumuunge mkono kuchukua nafasi ya Mkuu (Mbowe). Utangulizi huo (udhaifu wa Mbowe) unaoonesha kinagaubaga kwamba tunahitaji mabadiliko na hatua iliyofuata ilikuwa ni kuangalia nani anaweza kuleta mabadiliko tunayohitaji.
“Ni vema ikazingatiwa kwamba mtu ambaye tungemuunga mkono lazima awe mwenye uwezo mkubwa kuliko tunayetaka kumtoa (Mbowe). Awe ana sifa za kiuongozi na zaidi sana awe na uwezo wa kupambana na mkuu aliyeko.
“Katika kuchunguza ndani ya taasisi (Chadema), tuliridhika kwamba Mtendaji Mkuu Msaidizi (Naibu Katibu Mkuu, Zitto), ana sifa zote tulizozitaja hapo juu ingawa kila mwanadamu ana udhaifu wake.
“Ni dhahiri pia kwamba udhaifu wa Mtendaji Mkuu Msaidizi unarekebika kuliko wa mkuu aliyepo,” umeeleza mkakati ambao Dk Mkumbo amekiri kuuandaa na kusisitiza hajutii kazi hiyo aliyoiita ni ya matamanio ya mabadiliko ndani ya Chadema.
“Nasisitiza tena kwamba siamini hata kidogo kwamba matamanio ya mabadiliko ya
uongozi ndani ya chama, na kuandaa mikakati ya kufikia matamanio hayo kwa njia za kidemokrasia ni uhaini,” alisisitiza Dk Mkumbo alipokutana na waandishi wa habari Dar es Salaam kukiri kupanga kumuondoa Mbowe na uongozi wake madarakani.

*Udhaifu wa Mkuu
SOMA ZAIDI: HABARILEO ONLINE

0 comments:

Post a Comment