Monday, November 25, 2013

Sheria Ngowi Sasa ni Kimataifa

MBUNIFU mahiri wa mavazi nchini Sheria Ngowi amesema kuwa kwa sasa anatarajia kufungua maduka ya kazi zake nchini Kenya, Nigeria na Afrika Kusini ili kuongeza idadi ya wateja wake.
Ngowi ambae kwa sasa anasifika zaidi kutokana na umahiri wake wa kushona suti nzuri kwa staili tofauti huku akiwa amewavalisha watu mbalimbali maarufu hapa nchini.
Akizungumza na safu hii alisema kuwa ubunifu ni soko ambalo linatakiwa kufanyiwa uwekezaji wa hali ya juu kwa kuwa kwa sasa wau wengi wanapenda kuvaa nguo zilizobuniwa na wabunifu wa ndani.
Alisema kuwa katika nchi hizo kutakuwa na wawakilishi wake ambao watakuwa wakisikiliza mahitaji ya wateja na kisha kufanyiwa kazi.
Alisema kuwa analenga kuhakikisha kuwa kila mtu anavaa nguo zilizobuniwa naye.
Alisema kuwa atahakikisha kuwa iwapo mtu asipovaa suti inayotengenezwa naye basi atavaa tai, suruali au hata shati lenye kubuniwa na yeye.
Aliongeza kuwa suti yake moja anashonesha kwa kuanzia milioni hadi milioni nne na tano.
"Mimi kwa sasa nina mikakati ya kuhakikisha kuwa ninaongeza soko langu katika ubunifu na kuongeza wateja ikiwa pamoja na kuwakilisha watanzania katika sekta ya ubunifu nchini"alisema Ngowi.


0 comments:

Post a Comment