Wednesday, November 27, 2013

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA NCHINI, JOHN CASMIR MINJA AFUNGUA KIKAO MAALUM CHA KUPITIA RASIMU YA MABORESHO YA JESHI LA MAGEREZA LEO MKOANI MOROGORO

1Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini John Casmir Minja(wa tatu kushoto) akitoa hotuba fupi ya ufunguzi rasmi wa Kikao Maalum cha kupitia rasimu ya Maboresho ya Jeshi la Magereza pamoja na Mafunzo ya “Risk Management” katika Ukumbi wa Hoteli ya Edema, leo Novemba 27, 2013 Mkoani Morogoro. 2Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Jeshi la Magereza, Bw. Venance Nijimbere akiwasilisha Mada ya “Risk Management” kwa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza katika Kikao Maalum cha kupitia rasimu ya Maboresho ya Jeshi la Magereza kinachofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Edema, Mkoani Morogoro. 4 
Baadhi ya Washiriki mbalimbali wa Kikao Maalum cha kupitia rasimu ya Maboresho ya Jeshi la Magereza wakimsikiliza Mtoa Mada ya “Risk Management”(hayupo pichani) wakati akiwasilisha Mada hiyo. 5Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja( wa pili kulia) akiteta jambo na Makamishna wa Jeshi la Magereza baada ya kufungua rasmi Kikao Maalum cha kupitia rasimu ya Maboresho ya Jeshi la Magereza(wa kwanza kulia) ni Kamishna wa Huduma za Urekebishaji, Deonice Chamulesile(wa kwanza kushoto) ni Kamishna wa Fedha na Utawala, Gaston Sanga( wa pili kushoto) ni Kamishna wa Sheria na  Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa. Kikao hicho kitafanyika kwa siku tatu mfululizo katika Ukumbi wa Hoteli ya Edema, Mkoani Morogoro.
3Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja(wa tatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa Kikao Maalum cha kupitia rasimu ya Maboresho ya Jeshi la Magereza katika Ukumbi wa Hoteli ya Edema, Mkoani Morogoro mara baada ya ufunguzi rasmi(wa kwanza kulia) ni Kamishna wa Fedha na Utawala, Gaston Sanga(wa pili kulia) ni Kamishna Huduma za Urekebishaji, Deonice Chamulesile(katikati) ni Mkurugenzi wa Sera na Mipango Wizara ya Mambo ya Ndani, Bw. Haji Janabi(wa kwanza kushoto) ni Mkaguzi wa Ndani wa Jeshi la Magereza, Bw. Venance Nijimbere(wa pili kushoto) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa( wa tatu kushoto) ni Mtaalam na Mchambuzi wa maswala ya Utawala toka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bi. Veira Shoo( Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

0 comments:

Post a Comment