Wednesday, December 26, 2012

Barcelona Kutomuuza Villa

 
MKURUGENZI wa soka wa Barcelona, Andoni Zubizarreta amesisitiza kwamba mshambuliaji wao, David Villa anayewaniwa na Arsenal hatauzwa, kwani si utaratibu wao kuwauza wachezaji wao bora katikati ya msimu.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Hispania amekuwa akipigania kupata namba kwenye kikosi hicho, tangu alipopona majeraha ya mguu wake aliovunjika na sasa amehusishwa na mpango wa kuondoka klabuni hapo Januari.

Arsenal imekuwa ikitajwa kwamba inawania kumsajili Villa wakati wa dirisha dogo la usajili Januari, lakini sasa Barcelona imebainisha wazi kwamba haitamuuza.

“Januari tutaendelea kuwa na Villa na vizuri kuelewa kwamba Barcelona haina utaratibu wa kuwauza wachezaji wake bora wakati wa dirisha dogo la Januari,” amesema Zubizarreta akiiambia televisheni ya Canal Plus.

“David ni mchezaji ambaye analeta mabao kwa timu, hivyo hatuna sababu ya kumuuza.

“Na sasa amepona kabisa baada ya kuvunjika mguu na naamini kwamba sasa atarudi dimbani akiwa na ari kubwa mno ya kufunga mabao.”

0 comments:

Post a Comment