
Ofisa Mfawidhi Kanda ya
Mashariki wa Mamlaka ya Usafiri wa Nchikavu na Majini (Sumatra), Conrad Shio
alisema lengo la uamuzi huo ni kuondokana na tatizo la usafiri.
Alisema kuwa mabasi ambayo yalikuwa tayari kufanya shughuli
hiyo, yalitakiwa kupakia abiria wake kwenye Kituo cha Mabasi ya Mikoani cha Ubungo chini ya usimamizi wa
Sumatra na Polisi kwa kutumia bei halali iliyopangwa na Serikali.
“Kabla ya kuanza safari, mabasi haya yalitakiwa kuja ubungo na
kupakia abiria hapo chini ya usimamizi wa Polisi na Sumatra na baada ya hapo
tunawaandikia kibali na wanaanza safari yao,” alisema.
Aidha alisema katika operasheni waliyoianza ya kukagua mabasi
yanedayo mkoani na kudhibiti upandaji wa nauli kiholela kuanzia Novemba mpaka
Jumamosi iliyopita, mabasi 87 yalikamatwa kwa kosa la kupandisha nauli na
asilimia kubwa yalikuwa aina ya Toyota Double Coaster.
“ Katika mabasi tuliyokamata ni yale yanayofanya safari zake
Dar es Salaam-Moshi-Arusha, Dar es Salaam-Mwanza na Dar es Salaam-Bukoba.
“Lakini kwa asilimia kubwa ni mabasi ya Toyota Double Coaster badala
ya kufuata utaratibu tuliouweka na kuwa na vibali, waliweka vituo vyao Ubungo
Maziwa, Mwenge na maeneo mengi na hao ndio tuliowakuta na kosa la kupandisha
nauli hadi Sh 45,000,” alisema.
Alisema kuwa pia mabasi manne yanayofanya safari zake kutoka
ya Dar es Saalm kwenda Mwanza yamekamatwa kutokana na ubovu wa magari yao na
mengine zaidi yako katika orodha hasa baada ya kufuatiliwa mwenendo wao.
“Utakuta mabasi ya kampuni fulani, leo limeharibika hili,
kesho lingine na siku inayofuata lile la kwanza linaharibika, hii inaonesha
kuwa kampuni hiyo hayafanyi matengenezo. Majina ya kampuni hizo tutayataja
baada ya kuyafikisha makao makuu,” alisema.
Noah hapana
Shio alikana kuruhusu magari madogo aina ya Noah kusafirisha
abiria na kuonya kuwa magari hayo yatakuwa yakifanya hivyo kinyume cha sheria
na kwa kificho.
Kutokana na watu wengi kutaka kusafiri wakati huu wa msimu wa
sikukuu za mwishoni mwa mwaka, bei za nauli za kwenda mikoani zimepanda zaidi
huku baadhi ya abiria wakishindwa kusafiri kutokana na ongezeko la nauli na
mabasi kujaa.
Uchunguzi ulifanywa na gazeti hili, ulibaini kuwa bei ya
kutoka Dar es Salaam kwenda Arusha ilipanda hadi kufikia Sh 50,000 kwa abiria
mmoja ikiwa ni tofauti na bei ya Serikali ya Sh 16,400 kwa mabasi ya kawaida; semi-Luxury
Sh 25,100 na luxury Sh 28,600.
Gazeti hili lilibaini pia kuwa magari binafsi aina ya Noah
juzi yalisafirisha abiria kwenda Moshi na Arusha kutoka Dar es Salaam.
0 comments:
Post a Comment