Wednesday, December 26, 2012

Arsenal Yamuuza Arshavin

 
ANDREY Arshavin ameripotiwa kwamba atauzwa kwa pauni milioni 4 kwenda klabu ya Reading, wakati wa dirisha dogo la usajili Januari.
Arsenal imemruhusu mchezaji huyo wa kimataifa wa Urusi kuzungumza na klabu hiyo iliyopo mkiani mwa Ligi Kuu ya hapa na anatarajia kukamilisha taratibu zote wiki ya kwanza ya Januari.
Washika bunduki hao wameshafikia makubaliano na Reading juu ya ada na imeripotiwa kwamba atauzwa kwa pauni milioni 4.
Vyanzo vya habari vimeithibitishia tovuti ya goal.com kwamba, Arshavin ameshaichezea Arsenal mechi yake ya mwisho na anaondoka hapo wiki ya kwanza wakati wa dirisha dogo la usajili litakapofunguliwa.
Arsene Wenger ameruhusu kuuzwa kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31, ambaye hajaanza katika mchezo wowote msimu huu tangu alipoaanza kwenye mchezo wa Ligi ya mabingwa Ulaya Desemba 4 mwaka huu dhidi ya Olympiakos.
Awali klabu za Fulham na Zenit St Petersburg ambayo ni timu ya zamani ya Arshavin, zilikuwa zinawania saini yake, lakini sasa Reading ndiyo imeweza kumtwaa nyota huyo.

0 comments:

Post a Comment