Monday, December 2, 2013

Universal Pictures, wadai kifo cha Paul Walker ni pigo kubwa kwao



Kampuni ya utengezaji filamu ya 'Universal Pictures', ambao ndiyo wazalishaji wa mfululizo wa filamu za Fast & Farious imetoa neno baada ya kifo cha mwigizaji Paul Walker.

Sehemu ya taarifa uiliyotolewa na kampuni hiyo inasema, "Wote sisi ndani ya Universal tumepata mshituko mkubwa sana".

"Paul alikuwa ni mmoja ya watu ambao alikuwa anapendwa na kuheshimiwa ndani ya familia ya studio yetu kwa muda wa miaka 14, pigo hili si kwetu pekee bali kwa kila mtu ambaye ameshiriki filamu ya Fast & Farious, na mashabiki wote," alieleza sehemu ya taarifa hiyo.
Taarifa hiyo ya Universal iliongeza, "Tunatuma salama za rambirambi kwa dhati kabisa kwa familia ya Paul,".

Walker (40) ameacha binti wa miaka 15.

0 comments:

Post a Comment