Monday, September 9, 2013

Mwenge wazindua miradi ya bil. 19/- Temeke


Na Katuma Masamba
MWENGE wa Uhuru ulioingia wilayani Temeke juzi, ulitarajiwa kuzindua miradi 12 yenye thamani ya Sh bilioni 19 wilayani humo.
Akizungumza wakati wa kupokea mwenge huo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi, Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema alisema ni faraja mwenge huo unapoendelea kukimbizwa na kuzindua miradi kwani inaonesha jinsi Serikali inavyowajali wananchi wake. 
Mjema alisema miradi iliyotarajiwa kuzinduliwa na mwenge huo itawawezesha wananchi wa Temeke kupunguza adha waliyokuwa wakipata kutokana na kukosa baadhi ya mahitaji. 
"Mwenge unapoendelea kuwaka inaonesha jinsi Serikali inavyowajali wananchi wake katika shughuli mbalimbali ikiwemo za maendeleo, Watanzania ni mashahidi katika hili," alisema Mjema.
Awali Mkuu wa Wilaya ya Ilala, alisema katika wilaya yake mwenge huo umezindua jumla ya miradi tisa ambayo imegharimu Sh bilioni 2.2. Mwenge huo unatarajiwa kulala katika viwanja vya Zakhem, Mbagala kabla ya kukabidhiwa kwa Mkoa wa Lindi.

Ends

0 comments:

Post a Comment