8:02 AM
Na
Mwandishi Maalumu, Zanzibar
SERIKALI
ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imewahakikishia watumishi wa sekta ya afya kuwa
changamoto zinazowakabili, ikiwemo maslahi yao, zinatafutiwa ufumbuzi hatua kwa
hatua ili waweze kutoa huduma vizuri kwa wananchi.
Kauli
hiyo imetolewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali
Mohamed Shein jana wakati akifungua Chuo
cha Taaluma ya Sayansi za Afya kilichoko Mbweni, Wilaya ya Magharibi, Mkoa wa
Mjini Magharibi kisiwani Unguja.
Alisema
changamoto kubwa inayoikabili Serikali katika kutekeleza azma hiyo ni ukosefu
wa fedha jambo ambalo alikiri kuwa si kwa Serikali yake tu bali katika nchi
nyingi duniani.
Dk
Shein alisema Serikali itajitahidi kuhakikisha ajira kwa wanafunzi wanaohitimu
mafunzo katika sekta ya afya hazicheleweshwi na kwamba zitafanyika kwa
kuzingatia muundo wa utumishi kwa watumishi wa sekta hiyo.
Rais
wa Zanzibar alitangaza uamuzi wa Serikali wa kukiweka chuo hicho chini ya
Uongozi wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA).
Sambamba
na kutangaza uamuzi huo, Dk Shein ametoa mwito kwa Wizara na Uongozi wa Chuo
cha Afya kukubali mabadiliko vinginevyo watabaki nyuma wakati wengine wakisonga
mbele.
Naye
Waziri wa Afya, Juma Duni Haji alieleza kuwa kukamilika kwa ujenzi wa majengo
hayo matatu ambayo moja ni la darasa na mawili mabweni ya wanafunzi wa kike
kunadhihirisha namna hatua kwa hatua chuo hicho kinavyoimarika.
0 comments:
Post a Comment