KOCHA wa Italia Cesare Prandelli ameomba radhi kwa kusema
kuwa Mario Balotelli ni mchezaji pekee aliyeruhusiwa kutoka nje ya hoteli
Brazil kwa sababu ni mweusi.
Maofisa ulinzi
walikiambia kikosi hicho kwamba hawaruhusiwi kutoka nje ya hoteli wakati huu wa
michuano ya Mabara.
Prandelli alisema
mshambuliaji huyo wa AC Milan
aliruhusiwa kutoka nje ya hoteli kwa sababu: "rangi yake ni tofauti na
yetu,". Lakini baadaye akasema: "Samahani, ilikuwa ni utani".
Ilikuwa ni lazima
atoke kwa sababu mshambuliaji huyo wa zamani wa Manchester City Balotelli
alitakiwa kwenye hafla ya hisani kusaidia watoto waishio kwenye mazingira
magumu wa Salvador.
Awali tukio hilo
ilikuwa lifanyike Rio lakini ilibadilishwa na kuhamishiwa hapa, mahali ambapo
tuliambiwa hakuna anayeruhusiwa kutoka mbali na hoteli".
"Kabla
sijazungumza lolote kuhusu rangi ya ngozi... napenda kuweka wazi sababu za yeye
pekee kuruhusiwa kutoka nje ya hoteli".
"Alitoka, lakini
hakuwa na kazi nyingine ya kufanya zaidi ya kushiriki kazi ya hisani kwa ajili
ya watoto hao".
Italia jana usiku
ilitarajiwa kucheza na wenyeji Brazil kwenye Kombe la Mabara, mechi
iliyotarajiwa kuwa ya vuta nikuvute.
mwisho.
0 comments:
Post a Comment