CHAMA Cha Wamiliki wa
Mabasi Tanzania (TABOA), kimewashukia baadhi ya viongozi wa serikali hasa ngazi
za mikoa kuwa ni miongoni mwa wamiki wa magari aina ya Noah, ambayo hayana
uwezo wa kubeba abiria kwa mujibu wa sheria.
Mbali na hatua hiyo TABOA
imemuomba Waziri wa Uchukuzi Dk. Harrison Mwakyembe, kufanya ukaguzi maalum ili
kuweza kubaini hali ambayo imekuwa ikihujumiwa na viongozi hao kwa kupinga
agizo la Mamlaka ya Usafirishaji wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA).
Akizungumza na waandishi
wa habari Dar es Salaam jana Katibu Mkuu wa TABOA, Enea Mrutu, ilieleza kuwa
hatua ya viongozi wa serikali katika mikoa ya Kilimanjaro na Arusha ya kuungana
na wamiliki wa magari ya Noah inatia mashaka ikiwemo ya kutaka wabebe abiria
zaidi ya saba kinyume cha sheria.
Mrutu, alisema sheria ya
usafirisha iliyowekwa na SUMATRA imeweka wazi namna ya ubebaji wa abiri kwa
magari hayo ya abiria lakini baadhi ya viongozi wamekuwa wakiunga mkono hoja ya
kutaka gari hizo zitembe kilometa zaidi ya 50.
“TABOA inasikitishwa sana
na hatua ya hatua ya baadhi ya viongozi wa serikali ambao wameonekana wazi
kutaka kupinga sheria halali ya
SUMATRA ya namna ya kubeba abiria. Haiwezekani katika hili wao wawe mstari wa mbele katika hili la uvunjaji wa sheria hii halali.
SUMATRA ya namna ya kubeba abiria. Haiwezekani katika hili wao wawe mstari wa mbele katika hili la uvunjaji wa sheria hii halali.
“Ni wazi Noah hazina
leseni ya biashara lakini kwa Mkoa wa Arusha Mkuu wa Mkoa Magesa Mulongo ametoa
agizo magari haya yaruhusiwe kufanya safari zake sehemu zozote ile bila
kujali ya umbali na idadi ya abiria.
“Hata huko
zilipotengenezwa Japan mwisho wa kubeba ni watu saba iweje hapa Tanzania. Kuna
picha inayojengeka hapa kwani hata katika kikao kilichofanyika Juni 19, mwaka
huu mkoani Kilimanjaro wenye magari haya wamekuwa na jeuri kuliko SUMATRA kuna
nini hapa,” alisema na kuhoji Mrutu.
Katibu Mkuu huyo wa TABOA alisema
kuwa ruhusa iliyotolewa na Waziri Mwakyembe kuna baadhi ya viongozi wa ngazi ya
mikoa wanataka kuitumia vibaya huku wenye mabasi yanayobeba abiria kuanzia 10
hadi 65 wao wakiendelea kubanwa pekee.
Alisema vitendo vya
wabunge na baadhi ya wakuu wa mikoa kuunga mkono jambo hilo huku wakiwa na
shinikizo kubwa la kutaka watu hao kutokata leseni ni kwenda kinyume na sheria
za nchi.
“Ikiwa kwa Mkoa wa
Kilimanjaro hawa wenye Noah wanataka kuvunja sheria hali ya kuwa wamiliki wa
mabasi hatutakubaliana na hali hii hata
kidogo. Hivyo tunamtaka Waziri Mwakyembe aingilie jambo hili la
uvunjivu wa sheria kwa makusudi,” alisema.
kidogo. Hivyo tunamtaka Waziri Mwakyembe aingilie jambo hili la
uvunjivu wa sheria kwa makusudi,” alisema.
Mwisho
0 comments:
Post a Comment