WATU wawili akiwemo Mwenyekiti wa kitongoji cha
Ihumwa Kata ya Mtumba katika Manispaa ya Dodoma wamekutwa wakiuza nyama ya fisi
kwenye kilabu cha pombe za kienyeji.
Wanaotuhumiwa kuuza nyama hiyo ya fisi ni
Gabriel Mwaluko ambaye ni Mwenyekiti wa Kitongoji na Dickson Mafutaa aliyekuwa
akishirikiana na mwenyekiti huyo kuuza ‘kitoweo’ hicho.
Kukamatwa kwa watu hao kunatokana na taarifa za wananchi zaidi ya 10
walionunua na kula nyama hiyo na kuwa na
wasiwasi kutokana na kuuzwa kwa bei rahisi hali ambayo ilifanya wafikishe
taarifa hiyo kwa Ofisa Afya.
Akizungumzia tukio hilo la
Jumatatu mchana, Ofisa Afya wa Kata ya Mtumba, Michael Dong’o alisema mwenyekiti huyo
alikutwa akiwa ameweka nyama hiyo kwenye mifuko ya rambo na kuiuza kati ya Sh
500 hadi Sh 1,000 kwa kipande kimoja.
Dong’o alisema baada ya kumuhoji Mwenyekiti huyo, alisema nyama waliyokuwa wakiuza
ilitokana na fisi waliyemuua kutoka kwenye pori la Ihumwa.
Alisema waliamua kumchuna na kisha kukata
vipande vya nyama hiyo na kisha kupeleka kwenye kilabu cha pombe za kienyeji
kwa ajili ya kuuza.
Kwa mujibu wa ofisa afya, watuhumiwa hao
walikiri kuuza nyama ya fisi na wakati huo huo inadaiwa walikutwa na ngozi ya
mnyama huyo ikiwa imehifadhiwa kwenye mfuko wa plastiki.
Ofisa Afya anadai mwenyekiti huyo wa kitongoji
alisema kuwa licha ya kuuza nyama hiyo kilabuni, pia familia yake ilipata.
Afisa
afya aliwataka wakazi wa maeneo ya kuwa makini kwa kujihadhari na kula nyma zilizothibitishwa na wataalamu
wa afya.
Alisema ni vizuri kwa wananchi kuacha uchu wa
kula nyama hasa zinazouzwa kwenye vilabu
vya pombe vya kienyeji kuepuka magonjwa hatari yanayoweza kusababishwa na
nyama.
Kulingana na maelezo ya ofisa afya, wanakusudia
kuwafungulia watuhumiwa hao mashitaka polisi
kwa ajili ya uchunguzi zaidi na hata uhalali wa kuwa na nyama na ngozi
ya fisi.
0 comments:
Post a Comment