Monday, November 26, 2012

'BREAKING NEWZZZ' SHARO MILIONEA AFARIKI DUNIA KWA AJALI YA GARI


 
Msanii aliyejizolea umaarufu mkubwa kutokana na style yake ya uigizaji Hussen Ramadhani Mkiete (27) aka Sharomillionea amefariki dunia usiku wa kuamkia leo kwa ajali ya gari.
Akizungumza na Clouds Fm Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Constatine Masawe alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo kwa kusema msanii huyo alipata ajali hiyo majira ya saa mbili usiku maeneo ya Maguzuni Songa karibu na Wilaya ya Muheza.
Alisema msanii huyo alikuwa njiani kwenda kumuona mama yake na alipata ajali na gari aina ya Toyota Harrier lenye namba T478 BVR. Aidha alisema gari hilo ghafla lilitoka nje ya barabara hatimaye kupinduka na kufariki dunia papo hapo.
Hata hivyo RPC huyo alisema kuwa taarifa zaidi hazikuweza kupatikana kwa kuwa msanii huyo alikuwa peke yake ndani ya gari hilo. Mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitali Teule ya Wilaya ya Muheza.
Hili ni pigo linguine tena kwa tasnia ya filamu nchini kwa kuangalia ni siku chache tu kutokea kwa kifo cha Mlopela na hivi juzi tena kifo cha John Maganga anaetarajiwa kuzikwa leo na hivi leo tena msanii Sharo milionea.
Samber Junior inatoa pole kwa familia ya marehemu, wasanii wote wa filamu na muziki na  watu wote walioguswa na msiba huu. Mungu ailaze Roho ya marehemu Pema Peponi….Ameen.

0 comments:

Post a Comment