Thursday, March 1, 2012

FLAVIAN KUIBUKA NA PASTOR'S WIFE


MSANII wa filamu Esther Flavian, amesema kuwa anakamirisha kazi yake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Pastor’s Wife’, ambayo itakuwa sokoni wiki chache zijanzo.
Akizungumza kwa njia ya simu, msanii huyo amesema kuwa huo ndiyo ujio wa mpya kwa mwaka huu na kilichobaki katkika filamu hiyo ni kumalizia kuhariri ili iweze kwenda sokoni.
Aliongeza kuwa filamu hiyo itakuwa inahusu maisha ya mchugaji na mke wake pindi wanapokuwa nyumbani hivyo ni stori ambayo inataeleza maisha halisi yanavyokuwa kwa watu hao.
“Filamu iko tayari imekamilika hivyo nawasihi mashabiki wangu wakae mkao wa kuipokea kwa sababu itakuwa na matukio mengi ya kusisimua ambayo hayana mfano hivyo kazi kwao,” alisema.
Pia msanii huyo amewaomba mashabiki wake wote watakao itazama kazi hiyo watoe maoni yao ili kuweza kujua wapi wamekosea.

0 comments:

Post a Comment