Saturday, March 31, 2012

BOB JUNIOR KUACHIA ‘NICHUM’ KIDEONI

Raisi wa Masharobaro Bob Junior

RAISI wa masharobaro , Bob Junior, amebonga kuwa ile video ya wimbo wake wa ‘Nichum’, itakuwa hewani Jumatatu hii.
Akiongelea video hiyo msanii huyo alisema kuwa ni kazi ambayo imechukua muda mrefu hadi kukamilika hivyo anaamini itafanya vizuri kwani imetengenezwa katika ubora wa kimataifa tofauti na nyingine alizowahi kuzitoa hapoa awali.
Junior alisema kuwa ndani ya kichupa hicho amemtumia msanii wa filamu ‘Lulu’, ambaye naye ameonesha uwezo wa kupitiliza.
“Video ipo mashabiki wangu wataanza kuitazama kupitia televisheni mbambali, na naamini kwamba wataipokea vizuri kwa sababu ni kazi ambayo imeandaliwa katika kiwango cha kimataifa, in short ni moto wa kuotea mbali” alisema.

0 comments:

Post a Comment