Baada ya ‘Kisiwa
cha Malavidavi’ kufanya vizuri, Msanii wa muziki wa kizazi kipya bongo Z-Anto,
amesema kuwa baada ya ngoma hiyo, sasa anatarajia kutoa kazi mpya
inayokwenda kwa jina la ‘Super Star’.
Akichonga na
Samber Junior ,kuhusiana na kimya cha Msanii huyo, ambapo amedai kuwa kazi yake
hiyo anayotarajia kuiachia hivi karibuni itakuwa ni moto wa kuotea mbali.
Mbali na ujio wa
kazi hiyo pia amedai kuwa mwaka huu hafikili kutoa albamu kwani anatakuwa
akitoa ngoma moja moja ambazo anaamini zitasaidia kumuweka juu
ukiachilia mbali albamu.
“Kazi ipo katika mikono yangu kwa sasa ni hiyo, lakini baada ya wiki mbili nitakuwa katika mchakato wa kuitolea video hivyo naamini mambo yataenda vizuri tu,” Alisema.
“Kazi ipo katika mikono yangu kwa sasa ni hiyo, lakini baada ya wiki mbili nitakuwa katika mchakato wa kuitolea video hivyo naamini mambo yataenda vizuri tu,” Alisema.
0 comments:
Post a Comment