MSANII wa ndani ya
Bongo Movie Industry Skyner Ally ‘Skyner’,
amesema kuwa baada ya kucheza filamu nyingi za wasanii wenzake sasa anajipanga
kutoa filamu yake ambayo itakuwa na mastaa kibao wa tasnia hiyo.
Skyner alisema
kuwa tayari ameshacheza filamu nyingi za kushirikishwa hivyo anaamini iwapo
atasimama kuhahakikisha filamu yake inatoka itafanya vizuri sokoni.
Alisema filamu
yake hiyo kwa sasa bado hajaipa jina kwani yupo katika mchakato wa
kuangalia wasanii ambao wanaweza kucheza katika kiwango ambacho anahitaji
ingawa wapo baadhi ya nyota ambao majina yao yapo kichwani.
“Nimecheza sana filamu za watu hasa ‘Ray’, lakini kwa sasa nahitaji kusimama mwenyewe na kuonesha uwezo wangu, ingawa naamini itakuwa nzuri kwa sababu najipaga kuifanya iwe ni moja kati ya kazi zitakazofanya vizuri kimataifa,” alisema Skyner.
“Nimecheza sana filamu za watu hasa ‘Ray’, lakini kwa sasa nahitaji kusimama mwenyewe na kuonesha uwezo wangu, ingawa naamini itakuwa nzuri kwa sababu najipaga kuifanya iwe ni moja kati ya kazi zitakazofanya vizuri kimataifa,” alisema Skyner.
0 comments:
Post a Comment