Tuesday, February 28, 2012

MWASITI ATOKLEZEA SINGLE ILIYOMPA SHAVU LA KUTOSHA

Mwimbaji tkoa nyumba ya vipaji THT Mwasiti Almasi ‘Mwasti’amesema tangu aingie kwenye industry ya bongo fava huu ni mwaka wake wa tano huku akiwa na jumla ya single nane.
Mwasiti amesema katika nyimbo zote hizo zinazijulikana, katika kumbukumbu zake miongoni mwa nyimbo zilizomfanya kupata mialiko na show nyingi kuliko single zote ni wimbo wa ‘Nalivua Pendo’.
Aliyasema hayo kupitia kipindi cha Amplifier cha Millard Ayo kinachorushwa na Clods Fm.
“Millard hata nikifa kesho, kesho kutwa Nalivua Pendo kiukweli ni namba moja kwangu, ilinifanya nikakaa kimya muda mrefu sana na nikaendelea kupata hela, ina nipa showz mpaka kesho kutwa, japo Hao, sio kisa pombe, na Souljah nayo japo watanzania hawajaielewa sana ila zimechangia kunipa kipato”
Mwasiti amethibitisha pia kwamba single yake ya nalivua pendo, imempa asilimia 95 ya show zote alizowahi kufanya, ambapo ameitoa good news nyingine leo kwamba baada ya kuwa kimya kwa miezi zaidi ya saba, leo katoa single yake mpya inaitwa Kisima inayozungumzia mapenzi tu, amesimama kama mwanamke ambae amependa.
“kisima ni sehemu ambayo mahaba hayaishi kama unavyojua kisimani ni sehemu ambayo mtu anachota maji, ndio hivyo hivyo kwa kisima hiki mahaba hayaishi”

0 comments:

Post a Comment