
Mashabiki wa timu mbalimbali duniani kwa wiki moja
sasa wamekuwa wakivutana kila mmoja akitumia picha kama ushahidi kuwa
kiongozi huyo alikuwa akishabikia timu fulani.
Katika mitandao ya kijamii kama vile facebook,
twitter na instagram, mashabiki wamekuwa wakitumia ushahidi wa picha
mbalimbali ambazo kiongozi huyo alipiga na wachezaji kama kielelezo.
Kuishabikia Arsenal

Picha aliyopiga na wachezaji wa Arsenal wakiwa
uwanjani nchini Afrika Kusini mwaka 1993 inawafanya waamini kuwa shujaa
huyo alikwa akiishabikia Arsenal.
Shabiki mkubwa wa timu hiyo na mtangazaji wa kituo
cha televisheni cha CNN, Piers Morgan aliandika katika ukurasa wake
kuwa wamempoteza mtu muhimu katika klabu yako.
“Wakati dunia inasikitika kwa kumpoteza shujaa,
sisi mashabiki wa Arsenal tunasikitika kumpoteza shabiki mwenzetu
(Gunner),” aliandika Morgan.
Picha inayomuonyesha Madiba akiwa na wachezaji wa
Manchester United aliowaalika ofisini kwake mwaka 2006 imetumiwa na
mashabiki wa timu hiyo kama ushahidi wa madai kwamba alikuwa akiiunga
mkono timu hiyo.
Mashabiki hao wanasema isingekuwa rahisi kwa
Mandela kuacha shughuli zake na kuialika timu hiyo kama asingekuwa
anaipenda na kuishabikia.
Picha nyingine ya Mandela aliyopiga na kocha wa
timu hiyo, Alex Ferguson alipotembelea nchini Afrika Kusini mwaka
imetumika kama ushahidi kuwa kiongozi huyo alikuwa akiiunga mkono timu
hiyo.
Kuishabikia Liverpool


Mashabiki wa Liverpool wao ndiyo wamejihakikishia kabisa kuwa
Madiba alikuwa shabiki wa timu hiyo kwani katika historia yake hakuna
picha inayomuonyesha akiwa amevalia jezi nyingine ya mpira wa miguu
zZaidi ya Liverpool.
Wanasema Madiba kuna picha nyingi amevaa jezi ya
timu ya mpira wa miguu zaidi ya timu yao huku wakiwataka mashabiki wa
timu nyingine watoe ushahidi kama wao.

“Jezi ya timu usiyoipenda ni sawa na tambara chafu
la chooni, kamwe huwezi kuivaa , Madiba kuvaa jezi ya Liverpool ni
ishara kuwa alikuwa shabiki wa kufa na kuzikana (diehard fan),”
aliandika shabiki wa Liverpool katika mtandao wa facebook.
Wanasoka wajitoa mhanga
Wachezaji wa Didier Drogba na Emmanuel Eboue
wamenusuriika kupewa adhabu na Shirikisho la Mpira la Uturuki baada ya
kuonyesha ujumbe wa kumkumbuka Mandela.
Drogba baada ya mechi kwisha wiki iliyopita alivua jezi na kubaki na singlet iliyokuwa na maneno Rest iIn Peace Madiba.
Hata baada ya kutishiwa adhabu alisema hajutii na iwapo atapata nafasi nyingine atarudia kitendo hicho tena na tena.
Katika sheria za soka mchezaji haruhusiwi
kuonyesha maneno yanayohusiana na siasa, hata hivyo shirikisho hilo
lilishindwa kuwaadhibu baada ya mashabiki kuwaunga mkono.
Klabu ya soka ya Galatasaray nayo iliweka picha kubwa ya Mandela nje ya uwanja wao ujulikanao kama Turk Telekom Arena.
Mandela kupenda michezo
Mandela alikuwa mpenda mchezo, aliwahi kusema kuwa
michezo na siasa haviwezi kuchanganywa, lakini ni marafiki walioungana
kwa kiasi kikubwa, wenye urafiki wa karibu.
Kauli hiyo aliitoa Juni 24, 1995 aliitoa Mandela
jijini Johannesburg akiwa Rais wa Afrika Kusini alipokuwa akikabidhi
Kombe la Dunia la ‘Rugby’ kwa nahodha wa timu ya nchi hiyo, Springboks,
Francois Pienaar.
Soma Zaidi
Soma Zaidi









0 comments:
Post a Comment