Monday, December 9, 2013

KINANA AMALIZA ZIARA, APANDA TRENI YA TAZARA KUREJEA DAR.ALAKIWA KWA SHANGWE

 Katibu Mkuu wa CCM, Komredi Abdulrahman Kinana na Katibu wa NEC wa Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha Rose Migiro wakiteremka kwenye Treni ya Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) Stesheni ya Mlimba, mkoani Morogoro jana, tayari kwenda kuwasalimia wafuasi wa CCM pamoja na wananchi wakiwa safarini kutoka Makambako mkoani Njombe kwenda Dar es Salaam. Kinana na msafara wake walikuwa katika ziara ya siku 26 katika mikoa ya Mtwara, Ruvuma, Mbeya na Njomba kuimarisha uhai wa chama na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa kwa kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM.
 Kinana na Nape wakimwangalia Dk. Migiro akiteremka kwenye treni hiyo katika Stesheni ya Mlimba.
 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akiwa na Katibu wa CCM Kata ya Mlimba Selemani Balali  wakati msafara wa Kinana ulipoteremka kwa muda katika Stesheni ya Mlimba.

 Nape akiangalia samaki waliokuwa wakiuzwa katika stesheni la Mlimba, Kulia ni Dk. Migiro.
 Kinana, Migiro na Nape wakiwa na baadhi ya viongozi wa CCM Kata ya Mlimba alipotembelea Stesheni ya Mlimba.
 Komredi Kinana akiwa na Katibu wa CCM,Kata ya Mlimba Selemani Balali  alipokuwa akielekea kupanda treni katika Stesheni ya Mlimba, Morogoro kwenda Dar.
 Kinana akizungumza na baadhi ya wananchi katika Stesheni ya Mlimba
 Jopo la wanahabari wa Televisheni, magazeti, Redio na mitandao ya Kijamii (Bloggers), walioambatana na msafara wa Komredi Kinana  wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kuwasili salama katika Stesheni ya Dar es Salaam leo asubuhi.
 Kinana akilakiwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhan Madabida baada ya kuwasili salama katika Stesheni ya Dar es Salaam leo asubuhi.
 Dk. Migiro akilakiwa na Madabida
 Nape akikukbatiwa kwa furaha na madabida ya kuwasili Dar es Salaam  leo.
 Kinana akivalishwa skafu na Chipukizi alipowasili Dar es Salaam leo.
 Komredi Kinana, Nape Nnauye  na Dk. Migiro wakiwasalimia wafuasi wa CCM waliofika kuwalaki katika Stesheni ya Tazara, Dar es Salaam.
 Komredi Kinana akisalimiana na wafuasi wa CCM
 Dk. Migiro na Nape wakiimbiwa wimbo
 Madabida akihutubia wakati wa mapokezi hayo
 Nape akiwashukuru wanahabari waliombatana nao kwenye msafara katika ziara ya siku 26 katika mikoa minne.
 Kinana akihutubia na kutoa shkurani kwa mapokezi hayo pamoja na wanahabari alioambatana nao kwenye ziara hiyo, akiwemo mmiliki wa Blogu hii ya Kamanda wa Matukio, ambaye pia ni Mpiga Picha Mkuu wa gazeti la Jambo Leo, Richard Mwaikenda.
 Mwenyekiti wa Wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu (wa pili kulia) akiwa miongoni mwa wanaCCM waliofika kuulaki msafara wa Kinana.
 Kinana akiwashukuru wanahabari alioambatana nao kwenye ziara hiyo.
 Kinana akimkumbatia mtangazaji wa Redio Uhuru, Sheila Simba
 Nape akikukmbatiana na Mhariri wa Habari wa gazeti la Jambo Leo, Said Mwishehe
Kinana akimkumbatia mwandishi wa Kituo cha Televisheni cha Star, Joseph Mpangala. PICHA ZOTE NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA WA Blog ya Kamanda wa Matukio.

0 comments:

Post a Comment