Wanafunzi
hao walitoa kauli hiyo juzi wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wanafunzi wa
kike ambao ni viongozi wa mabaraza.
Walisema
sasa hakuna vipindi vya michezo ya ngoma za asili kutokana na Serikali kutoona
umuhimu wa kuwepo, hali inayowafanya kutofahamu mila na desturi za utamaduni wa
Mtanzania.
Asha
Hassani (13) wa Shule ya Msingi Chalula, alisema inasikitisha kuona Serikali
imekuwa ikisisitiza michezo mingine, lakini kwa upande wa ngoma za asili halipo
kabisa.
Alisema
michezo kama mipira na kukimbia imekuwa ikitengewa muda, lakini jambo kama hilo
halipo kwenye ngoma za asili.
Hata
hivyo, Ofisa Utamaduni Wilaya ya Chamwino, Nicholaus Achipota alisema tatizo
lililopo ni baadhi ya walimu kubadilisha vipindi vya ngoma za asili na kuweka
masomo mengine.
Awali,
wakizungumza kwenye kujadili suala hilo la utamaduni, walimu wa shule ya msingi
za Mvumi Misheni walisema kukosekana kwa vipindi hivyo vya ngoma za asili,
kunatokana na kutowekwa kwenye mtaala wa kufundishia masomo.
Walimu
Flora Kulwa na Shukrani Msambili walisema mfumo mzima wa serikali katika
michezo mashuleni umelenga zaidi kwenye masomo ya darasani. Walisema kwenye
ngoma za asili huwa na umuhimu pale ambapo kuna ugeni shuleni, lakini si
vinginevyo.








0 comments:
Post a Comment