
SASA ni dhahiri kwamba Chama Cha
Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinameguka na kubaki vipande, kutokana
na uamuzi uliochukuliwa jana na Kamati Kuu yake kuwavua rasmi madaraka
vigogo wake watatu. Mkutano wa siku mbili wa Kamati Kuu ya chama hicho
uliofanyika Dar es Salaam hatimaye jana ulimalizika kwa kuchukua hatua
dhidi ya Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe, Mjumbe wa Kamati Kuu, Dk
Kitilla Mkumbo na aliyekuwa Mwenyekiti wa Mkoa wa Arusha, Samson
Mwigamba.
Baada ya hatua hiyo ambayo ni ngumu
kuaminika ndani na nje ya chama hicho kikuu cha upinzani, zilipatikana
taarifa zingine za Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Bara, Said Arfi
kujiuzulu wadhifa huo. Kwa hatua hiyo, viongozi hao wamevuliwa nyadhifa
zao zote za uongozi ndani ya chama kutokana na tuhuma za kuunda mtandao
wa kukivuruga chama hicho na kuiagiza Kamati ya Chama ya Wabunge
kuchukua hatua za haraka kuhakikisha Zitto anavuliwa madaraka yake yote
ya Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.
Hayo yalibainishwa jana na Mwanasheria Mkuu wa chama hicho, Tundu Lissu alipokuwa akitoa uamuzi wa Kamati Kuu ya chama hicho.
Alisema uamuzi mwingine ni pamoja na
viongozi hao kuandikiwa hati zenye tuhuma dhidi yao haraka na watakiwe
kujieleza kwa nini wasifukuzwe chama kwa vitendo vyao, ikiwa ni pamoja
na kupewa fursa ya kujitetea kama inavyoelekezwa kwenye Katiba ya chama.
Lissu alisema Kamati pia imetaka baada
ya utekelezaji wa azimio, ikutane kwa kufanya uamuzi juu ya hatma ya
watuhumiwa na hatua zingine zitakazofuata.
Mtandao wa ushindi Akizungumza
kilichojiri katika mkutano huo hata kufikia uamuzi huo, alisema ilibaini
kuwapo mkakati wa kukiharibu chama kupitia waraka uitwao “Mkakati wa
Mabadiliko 2013” ulioandaliwa na kikundi kinachojiita “Mtandao wa
Ushindi”.
Alisema kikundi hicho vinara wake wakuu
ni wanne ambao ni Zitto anayejulikana kama ‘MM’ au Mhusika Mkuu, Dk
Mkumbo anayejulikana kama M1, Mwigamba anayejulikana kama M3 na mtu
mwingine ambaye jina lake halijajulikana anayejulikana kama M2.
Alisema M2 anatajwa kwenye waraka huo
kuwa yuko ukingoni kuondolewa katika mageuzi ya kiutendaji yanayoendelea
katika Sekretarieti ya Chama Makao Makuu. “Kwa mujibu wa waraka
wenyewe, mkakati huu umeandaliwa pamoja na M2 na M3 na kupitiwa na
kurekebishwa na M1 ili upelekwe kwa MM kwa maoni ya mwisho na kuanza
utekelezaji,” alisema.
Lissu alisema mbele ya Kamati Kuu, Dk
Mkumbo alikiri kuwa MM ni Zitto, M1 ni yeye na M3 ni Mwigamba na kukataa
kumfahamu M2 na kukiri yote yaliyoandikwa katika Mkakati wa Mabadiliko
2013 ni ya kwao.
Alisema lakini Zitto alikana kuuona
waraka huo na kumhusu kwa kuwa ametaja tu jambo ambalo Kamati Kuu
ilikataa kutokana na kuwa Juni 30 waraka huo ndio ulihaririwa mara ya
mwisho na kupelekwa kwa Zitto kwa ushauri na utekelezaji.
Lissu alisema mkakati huo ni wa
kuipasuapasua Chadema na kuiangamiza kabisa kwenye uso wa siasa za nchi
na si wa kufanya mabadiliko ya kiuongozi ndani ya chama kwa njia ya...
SOMA ZAIDI: HABARILEO ONLINE








0 comments:
Post a Comment