Friday, December 14, 2012

Watoto Waokota Bastola Iliyotupwa na Majambazi

BASTOLA iliyotengenezwa kienyeji imeokotwa na watoto wadogo katika uwanja wa Shule ya Msingi Ifumbo wilayani Chunya mkoani Mbeya ikiwa imetelekezwa.

Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Diwani Athuman alisema jana kuwa bunduki hiyo inayotumia risasi za shotgun iliokotwa Jumatano wiki hii saa 3:00 asubuhi.

Alisema watoto hao wa walikuwa wakicheza uwanjani hapo  ndipo walipoona mfuko wa plastiki uliofungwa na baada ya
kuufungua wakakuta bastola hiyo.

Kamanda Athuman alisema baada ya kubaini kuwa ni bunduki waliipeleka kwa wazazi wao ambao kuchukua jukumu la kuipelekea kwa uongozi wa Kijiji.

Wakati huo huo askari mgambo wa Kijiji cha Bitimanyanga wilayani Chunya wamekamata risasi 114 za bundukia aina ya  SMG  zilizotupwa na mtu anayehisiwa kuwa jangili.

Kamanda Athuman alisema risasi hizo pia zilikamatwa wiki  iliyopita saa 9:00 alasiri katika Hifadhi ya Lukwati kijijini hapo na askari mgambo Daimon John (32)  akiwa na wenzake wawili walipokuwa katika doria ndani ya hifadhi hiyo.

Alisema wakati wakiendelea na shughuli za ulinzi walimkurupusha mtu mmoja ambaye alikimbia na kutupa
mfuko aliokuwa ameubeba na ndani yake zilikutwa risasi hizo, nguo na redio ndogo.

0 comments:

Post a Comment