

Lile tamasha
kubwa kuliko yyote hapa nchini, maarufu kama Serengeti fiesta ambalo limekuwa
likizunguka mikoa ya Tanzania bara na kufikia takribani mikoa 11 sasa linaelekea
katika kilele chake katika viwanja vya leaders jijini Dar es Salaam siku tar 6
jumamosi mwezi huu ambapo msanii wa
hiphop kutoka nchini Marekani Leonard Roberts maarufu kama Rick Ross atatumbuiza katika tamasha hilo.
Akizungumzia
ujio wa msanii mkubwa kama huyo katika mahijiano maalum jijini Dar esSalaam
jana, meneja wa bia ya Serengeti bw. Allan Chonjo amesema tamasha la Serengeti
fiesta limekuwa likifanya vizuri sana katika mzunguko wake na kwamba watanzania
wamekuwa wakifurahia uwepo wa tamasha hilo kutokana na mafanikio mbalimbambali
ambayo wamekuwa wakipata kila ilpofika kipindi cha Serengeti fiesta “mwaka huu
tutakuwa na Rick Ross na kwamba watanzania waendelee kujenga imani na Serengeti
fiesta kwani kila kilele cha tamasha hilo kwa mwaka, ni mwanzo wa maandalizi ya
tamasha hilo kwa mwaka unaofuata.
Rick Ross
ambaye ni mmoja kati ya wasanii wanaotamba sana katika miondoko ya kurap (hip hop)
katika majukwaa ya matamasha mkubwa nchini marekani, atawasili hapa nchini siku
ya alhamisi tayari kabisa kutumbuiza katika maadhimisho ya kilele cha tamasha
la Serengeti fiesta siku ya jumamosi mwishoni mwa wiki hii.
Tamasha la
Serengeti fiesta linafikia hatua hiyo likitokea nyanda za juu kusini Mbeya na
Iringa mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo wasanii mabali mbali wa miondoko ya
bongo flava walishambulia jukwaa kwa nyakati tofauti na kuwatumbuiza vilivyo
mashabiki wa tamasha la Serengeti fiesta waliokuwa wamefurika katika viwanja
vya sokoine jijini mbeya na Samora mjini Iringa.
Wasanii
walioshiriki katika tamasha la Serengeti fiesta nyanda za juu kusini ni pamoja
na Inspector Haroun, Juma Nature, Roma Mkatoliki, Linah, Amini, Supa nyota
Serengeti fiesta 2012 na wengine.
Mashabiki na
wakazi wa jiji la Dar es Salaam wanatarijwa kuungana pamoja katika viwanja vya
leaders kushuhudia shamramshamra na burudani mbalimbali kutoka kwa wasanii
mbalimbali wa kizazi kipya huku wengi wao wakisubiria kwa hamu kubwa kumuona
msanii Rick Ross kwa macho yao wenyewe kwa kiingilo cha shilingi za kitanzani elfu
20000/= kwa wale watakaonunua tiketi zao mapema na elfu 25000/= kwa wale
watakaonunu tiketi getini.
Tamasha la
Serengeti fiesta hufanyika kila mwaka amapo mwaka jana Serengeti fiesta limleta
mmoja kati ya wasanii wakubwa nchini marekani Ludacriss ambaye alitumbuiza
katika viwanja vya posta kijitonyama jijini Dar esSalaam.
Ajira mbalimbali za muda na za kudumu zimekuwa
zikianzishwa kupitia Serengeti fiesta katika maeneo yote ambayo tamasha hilo
lilipata kupita zikiwemo kuibuliwa kwa wasanii chipukizi na baadaye kujitegemea
kimuziki, kujengeka kwa majina ya wasanii mbalimbali ambao hawakupata
kufahamika zaidi kwa mashabiki wa muziki pamoja na kuibuka kwa wasanii wa
filamu kupitia tamasha hili la Serengeti fiesta,linalodhaminiwa na kampuni ya
bia ya Serengeti kupitia bia ya Serengeti premium lagaer.
0 comments:
Post a Comment