
Tamasha la Serengeti fiesta 2012 leo linafikia tamati kwa
mwaka huu baada ya kutimua vumbi kwa takribani miezi miwili tangu kuanza kwake
na kufanikiwa kuangusha burudani yake katika mikoa 11 ya Tanzania bara zikiwemo
Kilimanjaro, Tanga, Musoma ,Shinyanga , Mwanza, Tabora, Singida,Mbeya , Iringa,
Dodoma na Morogoro.
Sura tofautitofauti za wasanii mbalimbali wa muziki wa
kizazi kipya na baadhi ya wasanii maarufu wa filamu za kibongo (bongo movie) zimekuwa
zikionekana kwa nyakati tofauti katika majukwaa mbalimbali ya tamasha hilo
katika mikoa mbalimbali hali iliowafanya mashabiki wa tamasha hilo kushuhudia
ukweli juu ya kauli mbiu ya mwaka huu unaosema ‘ Serengeti fiesta 2012 muonekano tofauti, burudani ileile’
Maadhimisho ya kilele cha tamasha hilo
yanatamatishwa usiku wa leo katika viwanja vya leaders club maeneo ya kinondoni
jijini Dar es Salaam ambapo msanii mmoja kati ya wasanii wenye miraba minne kutoka nchini Marekani Leonard Roberts maarufu kama Rick
Ross atasababisha muonekano tofauti wa Serengeti fiesta kuendelea kushika
hatamu pale atakapopanda katika jukwaa lililoandaliwa kwa namna ya tofauti na
ya kipekee kulioko miaka iliyopita.
Rick Ross
ambaye ni mmoja kati ya wasanii wakali wanaotamba katika ulimwengu wa muziki wa
rap (Hiphop) nchini Marekani amewasili usiku wa kuamkia leo katika uwanja wa
ndege wa Mwalimu Nyerere na kupokelewa na
waandaaji wa tamasha hilo kampuni ya Prime Time Promotions wakiongozwa na
Mkurugenzi wa Clouds Media Group Bw. Joseph Kussaga na Mkurugenzi wa Utafiti wa
Clouds Media Group Bw. Ruge Mutahaba pamoja nao mkurugenzi wa masoko wa Kampuni
ya bia ya Serengeti Bw. Ephraim Mafuru akiwa ameongozana na meneja wa bia ya Serengeti Bw. Allan Chonjo kutoka kampuni ya bia ya
Serengeti ambayo ndio mdhamini mkuu wa tamasha hilo kwa mwaka wa tatu sasa.
Akizungumza
kuhusu ujio wa mwanamziki huyo na mstakabali mzima kuhusu tamasha la Serengeti
fiesta mwaka huu,mkuruganzi wa utafiti wa clouds media group Bw. Ruge Muatahaba
amesema taratibu zote zimekamilika na kwamba maandalizi yote kuhusiana na
tamasha hilo yako katika hatua nzuri “ maandalizi yako vizuri kabisa na mambo
yanakwenda kama yalivyotarajiwa, watanzania watarajie kuona burudani ya aina
yake tofauti kabisa na miaka iliyopita” alisema Mutahaba huku akitoa shukrani
zake za dhati kwa kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar esSalaam Sulleimani
Kova kwa kumhakikishia ulinzi wa kutosha katika eneo la tukio na maeneo ya
jirani na kusema kuwa mbali na askari polisi pia watakuwepo askari mgambo
kutoka katika makampuni ya ulinzi kama Altimate
Security na mengineyo hali itakayowafanya watanzania wote watakaofika na kupita
katika maeneo yanayozunguka eneo la tukio kuwa katika hali ya usalama.
Kwa niaba ya
wadhamini wa tamasha hilo kampuni ya bia ya Serengeti, meneja wa bia ya
Serengeti Bw. Allan Chonjo amesema kilele cha tamasha hilo mwaka huu itakuwa na
sura mpya kabisa hali itakayoonesha kwa vitendo muonekano mpya burudani ileile
ya Serengeti fiesta 2012 “ watanzania wengi wamekuwa wakishuhudia muonekano
mpya wa tamasha hili katika mikoa yote ambayo tumeweza kupita na kwamba
muonekano huo tunatamatisha hapa jijini kwa kufanya kila kitu kilichozoeleka
miaka iliyopita kuwa katika hali nzuri na ya kuvutia zaidi” alisema Chonjo na
kuongeza kuwa wasanii watakaotoa burudani ukumbini hapo watajitikeza jukwaani
kwa staili tofauti na kufanya tamasha hilo kuwa kivutio kwa mashabiki wake.
Aidha Bw.
Chonjo amewataka watanzania wote kuwa wastaarabu katika tamasha hilo kwa
kufuata kanuni na taratibu zilizowekwa ili kuepusha madhara na matatizo
yanayoweza kepukika “tumeweka utaratibu mzuri wa kununua tiketi za kuingilia
kwa kuweka vituo karibu kona zote za jiji ili kuepuka vurugu na msongamano
getini wakati wa kuingia” aliongeza Chonjo na kumalizia kwa kuwataka mashabiki
wanywe kistaarabu.
Tamasha la
Serengeti fiesta leo lina fikia kilele chake kwa mwaka huu 2012 tayari kabisa
kuanzania kwa maandalizi ya tamasha hilo kwa mwaka ujao 2013.
0 comments:
Post a Comment