Thursday, September 6, 2012

UKISHINDANA NA WAKONGWE UTAUMIA...!! - FID Q


Msanii Farid Kubanda, ‘Fid Q’ a.k.a Ngosha ze Swagga Don, ametoa ushauri kwa wasanii wanaotaka umaarufu wasijifananishe na wale waliotangulia katika sanaa hiyo muda mrefu.
Akizungumza kwa hisia, Fid alisema wapo wasanii wazuri tu, lakini uwezo wao unashuka kutokana na kuanza kusimama kwa kujifananisha na wakongwe walioanza kusota muda mrefu.
Alisema wasanii wakongwe tayari wana mtaji mkubwa wa mashabiki, hivyo kamwe hawataweza kupondwa au kuonekana vituko kwasababu ya wasanii wachanga wanaoingia na kutoka.
“Wasanii wachanga wakaze buti, lakini wasidharau kaka zao, maana tayari hao wana mtaji mkubwa wa mashabiki, hivyo hawawezi kuwa kama wao"...
“Wakifanya hivyo wataanguka na kupoteza thamani yao, maana Fid Q nimeanza kitambo na uwezo wangu umeshaonekana kuwa ni mkali na naweza kuhimili vishindo vya muziki wa Hip Hop nchini,” alisema Fid Q.
Fid Q ni miongoni mwa wasanii wanaofanya vyema katika tasnia ya muziki wa Hip Hop nchini, akiweza kukaa kileleni kwa miaka mingi sasa.

0 comments:

Post a Comment