Wednesday, May 14, 2014

Pombe inaua mtu mmoja kila sekunde 10 - WHO

IMEELEZWA kuwa pombe inaua watu milioni 3.3 kila mwaka duniani kote, ikiwa ni zaidi ya Ukimwi, Kifua Kikuu pamoja na magonjwa mengine, Shirika la Afya Duniani (WHO) limetoa taarifa hiyo siku ya Jumatatu na kuonya kuwa unywaji wa pombe na matumizi ya kilevi yanazidi kuongezeka.
“Hii kwa kweli inamaanisha kuwa kila ndamni ya sekunde 10 kuna kifo kinatokea,”  Shekhar Saxena, ambaye ni mkuu wa Idara ya magonjwa ya Akili na madawa ya kulevya wa WHO, aliwaambia waandishi wa habari Jijini Geneva.
Matumizi ya kilevi yalisababisha vifo milioni 3.3 kwa mwaka 2012, ambapo WHO wamesema kuwa ni sawa na asilimia 5.9 ya vifo vyote (asilimia 7.6  kwa wanaume na 4.0 ni wanawake)
Ikilinganishwa na HIV/AIDS ambayo inaua kwa asilimia 2.8, Kifua Kikuu kinasababisha vifo kwa asilimia 1.7 na magonjwa mengine kwa asilima 0.9, kwa mujibu wa utafiti uliofanywa.
"Mbinu za ziada zinahitajika kuwalinda watu kutoka athari za matumizi hasi ya pombe kwa afyaMahitaji,” Oleg Chestnov ambaye ni daktari wa Shirika hilo alisema katika taarifa yake wakati wa uzinduzi wa utafiti wa ripoti kubwa juu ya matumizi ya pombe na madhara yake kwa afya ya umma.
Matumizi mabaya ya pombe huwafanya watu kuugua magonjwa mbalimbali ikiwemo saratani, kifua kikuu, HIV na Pnemonia, ilieleza taarifa hiyo.
Vifo vingi vinavyotokana na matumizi ya pombe, karibu robo tatu husababishwa na magonjwa ya moyo na kisukari.
Ulevi wa pombe kupindukia na kuharibu afyav unakadiriwa kuwa ni asilimia 16 katika dunia nzima.
Wakati watu katika mataifa tajiri zaidi duniani , katika nchi za Ulaya na Marekani, n wanyawaji kuliko watu walioko katika nchi masikini bado hali ya uchumi wao inaonekana kupanda na hivyo kusababisha matumizi ya pombe kuongezeka.
Lakini mbali na kila mtu duniani kuwa mlevi, inaelezwa karibu nusu ya watu wazima wote duniani kamwe hawajagusa pombe na karibu asilimia 62 walisema hawajagusa wala kunywa kwa mwaka uliopita, ripoti hiyo ilionyesha.
Chanzo Daily Nation

0 comments:

Post a Comment