Friday, December 6, 2013

Mandela kuzikwa kijijini kwake Qunu siku ya Jumapili Desemba 15, 2013


Rais Jacob Zuma ametangaza muda mfupi uliopita kwamba mazishi ya Nelson Mandela yatafanyika siku ya Jumapili, Desemba 15 kijijini kwake Qunu, katika jimbo la Eastern Cape.
Rais Zuma pia ametangaza siku 10 za maombolezo kitaifa na bendera zitapeperushwa nusu mlingoti katika muda wote huo.
Aidha ameitangaza siku ya Jumapili ya Desemba 8, 2013 kuwa siku maalumu ya kitaifa ya maombolezo na kumkumbuka Madiba nchi nzima.
 Tayari msisimko wa mazishi hayo yanayotarajiwa kuwa ya kihistoria umekamata dunia nzima, ambapo tayari Rais Obama wa Marekani, mstaafu Bill Clinton na Waziri Mkuu wa UingerezaDavid Cameronni baadhi ya viongozi ambao wamethibitisha kushiriki.
Sala ya mazishi imepangwa kufanyika katika uwanja wa Taifa wa FNB Desemba 10, 2013 jijini Johanesburg.
Mwili wake utawekwa katika jengo la serikali liitwalo Union Buildings kuanzia Desemba 11 hadi 13 kwa kupewa heshima za mwisho, kabla ya kabla ya kupelekwa kijijini Qunu kwa ajili ya mazishi.
Uwanja wa Taifa wa michrezo wa FNB ambako sala rasmi ya Kitaifa ya mazishi itafanyika Desemba 10, 2013

Jengo la Union Buldings ambapo mwili wake utawekwa hapa kwa ajili ya kupewa heshima za mwisho kuanzia Desemba 11 hadi 13, 2013.

Ulinzi mkali katika nyumba ya familia ya Madiba kijijini kwake QUnu ambapo atapumzishwa katika nyumba yake ya milele Desemba 15,2013.

0 comments:

Post a Comment