Naibu
Waziri wa Kazi na Ajira Mhe,Makongoro Mahanga akitoa hotuba yake.
Huu
ndio mtandao uliozinduliwa

Wanafunzi
na wahitimu wa vyuo mbalimbali wakiwa kwenye kongamano la siku mbili jinsi ya kuandika barua ya maombi
ya kazi katika ukumbi wa Mw. Julius Kambarage Nyerere jijin
dar es Salaam.

Naibu
Waziri wa Kazi na Ajira Mhe Makongoro Mahanga, akimsikiliza Kaimu Mtendaji Mkuu
wakala wa Huduma za Ajira Tanzania (TaEsA), Boniface Chandaruba. Akielezea kazi wanazofanya kuhusiana na ajira
kwa vija mara baada ya kutembelea banda hilo,
Mratibu wa kitaifa shirika la Kazi Duniani (ILO),
akimuelezea Naibu Waziri wa Kazi na Ajira Mhe Makongoro Mahanga kuhusiana na
kazi wanazofanya kwenye shirika hilo.
Wafanyakazi wakala wa Huduma za Ajira Tanzania (TaEsA), wakiwa kwenye picha ya
pamoja,katika kongamano
la siku mbili jinsi ya kuandika barua ya
maombi ya kazi katika ukumbi wa Mw. Julius Kambarage Nyerere jijin
dar es Salaam.
Naibu
Waziri wa Kazi na Ajira Mhe Makongoro Mahanga, akiwa kwenye picha ya pamoja na Wanafunzi na wahitimu wa vyuo
mbalimbali pamoja na viongozi wengine.
SERIKALI imezindua mfumo maalumu wa kielektroniki wa taaifa
za soko la ajira, ambao utamuwezesha mtafuta kazi kufahamu nafasi mbalimbali za
kazi zinazotangazwa ndani na nje ya nchi.
Mtandao huo ambao umeelezwa kuwa utakuwa msaada mkubwa hususani
kwa vijana utamuwezesha muomba kazi kuomba nafasi hizo moja kwa moja katika
makampuni husika kulingana na vigezo vitakavyokuwa vikihitajika.
Akizundua mtandao pamoja na maonyesho ya shughuli za huduma za
ajira jana jijini Dar es
Salaam, Naibu Waziri wa Kazi na Ajira Makongoro Mahanga alisema, mbali na
kutangaza nafasi za ajira pia mfumo huo utawawezesha watu wenye nia ya kuwekeza
hapa nchini kutambua aina ya ujuzi unaopatikana nchini na kuwarahisishia
katika kuajiri.
"Hii itapunguza waajiri kuajiri wageni zaidi katika zile
nafasi ambazo zina wataalumu nchini kutokana na kufahamu mapema. Pia kwa
wanafunzi wqa vyuo vikuu watafahamu mapema ujuzi na taalumu wanazopaswa kusoma
kwa kuwa utatoa taarifa zitakazowezesha mtu kujua mahitaji ya sasa na ya siku
za usoni katika soko la ajira," aliongeza.
Kwa upande wa waajiri mfumo huo utawawezesha kutangaza nafasi za
kazi walizonazo ikiwa ni pamoja na sifa za mtafuta kazi wanayemuhitaji.
"Wataweza kupata wafanyakazi wenye viwango wanavyovitaka kwa urahisi kwa
kujiunga na mtandao huu," alisema.
Alisema hatua ya mtandao huo utasaidia kupunguza ukosefu vwa
ajira kwa vijana kwani kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2006 tatizo la ukosefu wa
ajira kwa vijana lilikuwa kwa asilimia 13.4 hivyo ni matarajio kiwango hicho
kitapungua baada ya waajiri wengi kutangaza ajira kupitia mtandao huo.
Mahanga ametoa wito kwa waajiri wote nchini kutumia mfumo huo
kutangaza ajira na watafuta kazi na kuutumia kupata taarifa sahihi ili kuweza
kuomba nafasi hizo.
Mtandao huo ambao umezinduliwa ni www.ajiralmis.go.tz, vijana wametakiwa
kuutumia kwa usahihi zaidi ili kunufaika na ajira zinazotangazwa.










0 comments:
Post a Comment