
Balozi
mpya wa kinywaji baridi cha Pepsi, Kala Jeremiah amesema juhudi zaidi ndiyo
zimeweza kufanikisha mpaka yeye kufikia hatua ya kukubalika na kampuni hiyo na
kusaini mkataba mnono wa kuwa balozi wa kinywaji hicho.
Kala
alifunguka kinamna kwenye 255 ya XXL ya Cloud Fm jana, ambapo alisema licha ya
juhudi zake lakini pia mashabiki wake wamekuwa ni mchango mkubwa katika
kufanikisha kupata mkataba huo.
"Unajua
hata wao (makampuni) wanapoangalia huwa hawachukui mtu kwa kuangalia kile
unachofanya tu, huwa wanaangalia pia jamii inakukubali vipi na wewe mwenyewe unajiheshimu kiaje, so katika hilo
nashukuru mafans wangu ambao wamekuwa wakinikubali muda wote" alisema
kala.
Aidha Kala amesema pia kwa kiasi kikubwa vyombo vya habari vimekuwa mbele kumpigania kuhakikisha kuwa anafahamika katika jamii na kampuni kubwa kama hizo.
Hata hivyo kala alikataa kutaja kiasi cha fedha anacholipwa baada ya kusaini mkataba huo.
Aidha Kala amesema pia kwa kiasi kikubwa vyombo vya habari vimekuwa mbele kumpigania kuhakikisha kuwa anafahamika katika jamii na kampuni kubwa kama hizo.
Hata hivyo kala alikataa kutaja kiasi cha fedha anacholipwa baada ya kusaini mkataba huo.
0 comments:
Post a Comment