CHAMA CHA MUZIKI WA KIZAZI
KIPYA TANZANIA (TUMA)
TAARIFA KWA VYOMBO
VYA HABARI 14-6-2013
Chama cha muziki wa kizazi
kipya Tanzania (TUMA) kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha
aliyekuwa msanii mahiri wa Hip Hop nchini marehemu Langa Kileo. Kwa mujibu wa
taarifa kutoka kwenye vyombo vya habari,marehemu Langa Kileo alifariki siku ya
jana jioni katikia Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alipopelekwa kwa ajili ya
matibabu. Tasnia ya muziki nchini imepata pigo lingine tena kwani ni takribani
muda wa wiki 2 tokea msanii mwingine mahiri Albert Mangweha afariki Dunia akiwa
nchini Afrika Kusini na kuzikwa katika Makaburi ya Kihonda yaliyopo Mkoani Morogoro.
Tunapenda kutoa wito kwa
wasanii wote nchini kujitokeza kwa wingi na kuonyesha upendo wa pamoja na kutoa
ushirikiano katika kipindi hiki kigumu cha msiba wa msanii mwenzetu Langa
Kileo.
Chama kinatoa pole kwa familia
ya marehemu, ndugu, jamaa, marafiki na mashabiki wote wa muziki nchini na
kuahidi kutoa ushirikiano katika wakati huu mgumu kweto sote.
Tunaamini tulimpenda lakini
Mungu alimpenda zaidi, Mungu ampumzishe kwa amani marehemu Langa Kileo.
Amin.
Fredrick
Gerson Mariki
Mwenyekiti wa TUMA (TANZANIA
URBAN MUSIC ASSOCIATION)







0 comments:
Post a Comment