Tuesday, January 29, 2013

UNDER THE SAME SUN YATOA VYETI KWA WAHITIMU WALIOSOMESHWA NA SHIRIKA HILO

Mwenyekiti wa IPP Bw Reginald Mengi (kushoto) akiwa katika picha ya Pamoja na Mhitimu wa Stashahada ya Uandishi wa habari Bi, Christina William Silas kulia ni Mkurugenzi na Muhasisi wa UTSS Canada na Tanzania Bw Peter Ash.
 
Peter Ash akikabidhi Cheti kwa Mmoja wa wahitimu katika Hafla hiyo.


Shirika lisilo la Kiserikali la kutetea watu wenye Ulemavu wa Ngozi (Albino)  Under  The Same Sun (UTSS) limetoa Vyeti  kwa walemavu wa Ngozi  43 waliohitimu ngazi mbalimbali za Elimu kwa kusomeshwa katika vyuo mbalimbali na Shirika hilo.

Akizungumza katika Hafla ya Utoaji wa Vyeti hivyo iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam nchini Tanzania,  Mwenyekiti wa IPP Bw Reginald Mengi ambaye ndiye aliyekuwa Mgeni Rasmi, amewapongeza wahitimu hao kwa kuhitimu na kuwataka kujiamini na kuamini kuwa na wao wanaweza wakiwa mahali popote.

Bw, Mengi pia amewapongeza sana Shirika hilo kwa kuwasomesha walemavu wa Ngozi kwani wamewapa ujasiri wa kujiamini kuwa wanaweza kufanya lolote katika jamii na jamii ikawakubali.

“Unatakiwa ujikubali kuwa nawewe unaweza na unaweza ukawa namba moja kati ya watu wengi, binafsi nawapongeza sana UTSS kwa kuwawezesha walemavu wa Ngozi kupata Elimu bora “amesema Dk Mengi.

Katika Warsha hiyo iliyofanyika leo katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam Baadhi ya Makampuni ilijitolea kuajiri wahitimu 20 ambao walikuwa tayari kupata Ajira kwani wengine waliopata vyeti bado wanaendelea na masomo yao.

Aidha, Muasisi wa Shirika hilo Peter Ash, alielezea changamoto mbalimbali na jinsi Albino wanavyohitajiwa kusaidiwa na kupewa nafasi katika jamii. Alisema wahitimu hao watakuwa ni mfano kwa watu wengine kuonyesha kuwa ikiwa watawezeshwa nao pia wanaweza.

Wahitimu wakiwa kwenye Picha ya Pamoja na Mgeni Rasmi pamoja na Uongozi wa UTSS.

Mkurugenzi na Muhasisi wa UTSS Canada na Tanzania Bw Peter Ash akiwapongeza wahitimu katika Hafla hiyo.

Waajiri kutoka katika Makampuni mbalimbali waliojitolea kuwa ajiri wahitimu hao

Mwanamuziki mlemavu wa Ngozi Ras Six akitoa Burudani katika Hafla hiyo

0 comments:

Post a Comment