Tamasha
la Mitikisiko ya Pwani lilianza mwaka 2004 katika ukumbi wa Traventine, mwaka
2008 lilifanyika Msasani club, mwaka 2009 likafanyika P.T.A. Hall iliyoko ndani
ya viwanja vya Mwalimu Nyerere Kilwa road, mwaka 2010 likafanyika Diamond
Jubilee Hall na mwaka 2011 likafanyika tena P.T.A. Hall....>>>
Mwaka huu 2012,
tamasha la Mitikisiko ya Pwani linafanyika ukumbi wa Dar Live tarehe 3/11/2012
siku ya Jumamosi. Tamasha litafungua milango saa nne asubuhi. Awamu hii itakuwa
ni kwa watoto na watu wazima ambao ambao wako mbali na jiji au wale ambao hawana
rukhsa kutembea usiku. Na kiingilio kwa awamu hii ni shilingi 5,000/= kwa
wakubwa na watoto shilingi 3,000/=, watapata burudani kutoka katika kundi
maarufu la Wanne Star.
Awamu
ya pili itaanza saa mbili usiku hadi majogoo kwa kiingilio cha shilingi
10,000/= tu. Awamu hii itapata burudani kutoka kwa bendi zipatazo 13 za taarab
ambazo ni Diamond Taarab Kutoka Zanzibar, Manuari, T. Moto, Zanzibar Njema, New
Zanzibar Modern Taarab, Kings Modern Taarab, jahazi Modern, East Africa Melody,
Dar Modern Taarab, Coast Modern Taarab, Five Star Modern Taarab, Jahazi Modern,
Mashauzi Classic na Bibie Khadija Kopa, WAUTAKAAA! KIAFRIKA ZAIDI…!







0 comments:
Post a Comment