Mama
wa Mitindo nchini Tanzania, Asia Idarous kupitia Kampuni yake ya Fabak Fashions
wanakuletea onyesho kubwa la Khanga za Kale litakalofanyika Novemba 23, 2012
katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.....
Onyesho
hili kubwa ambalo limekuwa likifanya vizuri kwa takribani miaka minne sasa na
kupata mafanikio makubwa ndani na nje ya Tanzania hasa katika nchi ya Marekani,
litawakutanisha wabunifu zaidi ya 30 kutoka nchi mbalimbaliambao wataonyesha
mavazi yao waliyoyabuni.
Watu
maarufu hapa nchini watapanda jukwaani siku hiyo kuonyesha mavazi ya khanga za
kale kutoka kwa mama wa mitindo, Asia Idrous Khamsin ambapo fedha
itakayopatikana kutona na onyesho hilo imepangwa kupelekwa katika kituo cha
watu walioathirika na madawa ya kulevya kilichopo Kikale, wilayani Rufiji Mkoa
wa Pwani.







0 comments:
Post a Comment