Nyota
wa ngoma ya ‘Nichumu’ ambaye pia ni bosi wa lebo ya Sharobaro Record,
ya jijini Dar, Bob Junior amesema sasa yuko tayari kusimama kwenye
ngoma moja na mkali kutoka Wasafi Entertainments, Diamond Platinumz.
Akizungumza
na teentz.com, mapema leo Bob Junior amesema licha ya kuwa
aliwasiri jana jioni kutoka Oman alikokuwa kwa mapumziko na
amepata bahati ya kuisikiliza ngoma mpya ya Diamond na kuona
kuwa ni kawaida kwani haina kitu kipya ilichofanyiwa
"Unajua kwa sasa mimi nimewapisha
vijana wangu kwanza watoa ngoma zao na baada ya wiki mbili nitatoa ya
kwangu, ninachoweza kusema ni kuwa sasa niko tayari kusimama kwenye wimbo
mmoja na dogo huyo kwani naamini mimi ni mkali zaidi yake na
watanzania wanajua hilo" alisema Bob.
Akiendelea zaidi Bob aliyeitikisa
Bongo kwa ngoma kali ya Oyoyo alifunguka kuwa, sasa ana mipango ya
kufanya vitu tofauti vitavyosukuma mbele muziki wa kizazi kipya na
zaidi akilenga katika kujiongezea mapato tofauti na kutegemea
MKWANJA WA shoo au promo za matangazo.







0 comments:
Post a Comment