Saturday, March 31, 2012

HAMMER Q AJIUNGA NA OFFSIDE TRICK


MKALI wa miondoko ya Taarab Hammer Q ametangaza kujiunga rasmi na kundi linalofanya  muziki wa mduara la Offside Trick.
Hammer Q amesema amechukua uamuzi huo wa kujiunga na kundi hilo baada ya msanii wa kundi hilo Muda Criss kupumzika kufanya muziki, hivyo yeye kuziba nafasi hiyo.
Aliongeza kuwa mipango yake ya kumiliki band bado iko palepale, na hata Offside Trick yupo kwa muda tu.
“Kwa sasa niko Offside Trick kwa muda tu, kundi hili limenichukua ili niweze kuziba nafasi ya Muda Criss kwa kuwa yeye ameamua kupumzika, na mipango yangu ya kumiliki band yangu binafsi bado iko palepale” alisema Hammer Q.
Aidha aliongeza kuwa bado anaona ni sawa kujiunga na wakali hao wa mduara kwa kuwa anaweza kufanya muziki wa aina yoyote, kitu ambacho kinatofautisha kati ya msanii na mwanamuziki.
“Mimi ni mwanamuziki na sio msanii kwa sababu naweza kuimba muziki wa aina zote, kwa hiyo hata kuwepo hapa Offside Trick bado nafurahia” aliongeza.
Hammer Q amewahi kutamba kusikika kupitia miziki ya aina ya tofauti ikiwemo aliyofanya kwa staili ya bongo fleva, Taarab na mduara.

0 comments:

Post a Comment