Jon Myuzik |
MSANII wa muziki
wa kizazi kipya nchini Jon Myuzik, amesema anafikiria
kucheza filamu lakini siyo za mapenzi kama ilivyo kwa wasanii wengine
ambao wengi hawana mabadiliko katika kazi zao wanazocheza.
Jon alisema anaweza kucheza filamu lakini
hatofanya kazi na nyota ambao wanamaringo kwa mafanikio yao
waliyoyapata, na anaamini kazi hiyo haina mwenyewe lakini wapo wasanii
wanaofanya vizuri.
“Nitafanya kazi hii ambayo hivi sasa ina idadi kubwa ya wasanii ambao wengi wao wanauza sura, bila kujua Watanzania wanahitaji nini hasa kipindi hiki ambacho kuna matatizo katika jamii zetu,” alisema Jon.
Jon alisema hata hivyo tayari ameshaanza mazungumzo na baadhi ya wasanii ambao anaamini wataweza kucheza katika filamu yake ya kwanza.
“Mazungumzo yanafanyika na baadhi ya wasanii ambao naamini nitaweza kucheza nao, lakini kabla ya yote lazima kwanza wanipe kwanza mfumo wa filamu unavyokuwa,” Aliongeza Jon.
“Nitafanya kazi hii ambayo hivi sasa ina idadi kubwa ya wasanii ambao wengi wao wanauza sura, bila kujua Watanzania wanahitaji nini hasa kipindi hiki ambacho kuna matatizo katika jamii zetu,” alisema Jon.
Jon alisema hata hivyo tayari ameshaanza mazungumzo na baadhi ya wasanii ambao anaamini wataweza kucheza katika filamu yake ya kwanza.
“Mazungumzo yanafanyika na baadhi ya wasanii ambao naamini nitaweza kucheza nao, lakini kabla ya yote lazima kwanza wanipe kwanza mfumo wa filamu unavyokuwa,” Aliongeza Jon.
0 comments:
Post a Comment