
MWENYEKITI Mtendaji wa Kampuni za IPP
Limited, Dk Reginald Mengi amekanusha kumiliki eneo kubwa la migodi.
Akizungumza jana, Mengi alisema eneo analomiliki kwa ubia na Watanzania
wenzake ni mgodi mmoja wa uchimbaji wa madini ya tanzanite lisilofikia
hata kilometa moja ya mraba.
“Desemba 8 mwaka huu, alipokuwa anajibu
swali la Tundu Lissu kuhusu ni nani anamiliki migodi ya Tanzania, Waziri
wa Nishati na Madini, Profesa Muhongo (Sospeter) alitoa takwimu za
kunihusu ambazo si sahihi.
“Ukweli ni kwamba mimi namiliki kwa ubia
na Watanzania wenzangu mgodi mmoja wa uchimbaji wa madini ya tanzanite
wenye eneo lisilofikia hata kilomita moja ya mraba na siyo Dar es Salaam
3 kama alivyosema.”
Dk Mengi alisema Waziri Muhongo amekuwa
akitoa taarifa kama hizo mara kadhaa ikiwemo pia wakati wa Mdahalo wa
rasilimali uliofanyika Desemba 8, mwaka huu katika Ukumbi wa Nkrumah,
Dar es Salaam ambapo Profesa Muhongo alitoa takwimu zinazoonesha Dk
Mengi anashika nafasi ya tatu ya Watanzania wanaomiliki maeneo makubwa
ya uwekezaji.
Profesa Muhongo alisema, Mengi anamiliki
eneo ambalo ukubwa wake ni mara tatu ya ukubwa wa Dar es Salaam na kuwa
hana cha maana anachonufaisha Watanzania na badala yake kujinufaisha
mwenyewe.
SOMA ZAIDI: HABARILEO ONLINE








0 comments:
Post a Comment