Naibu Waziri wa Wizara ya
Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi , Wizara hiyo, Benedict Ole Nangoro, amesema
utafiti umebaini ulaji wa nyama kwa mtanzania ni wastani wa kilo 12 kwa mwaka
tofauti na kiwango kilichopendekezwa na Shirika la Chakula la Umoja wa Mataifa
wa ulaji wa Kilo 50 kwa mtu kwa mwaka.
Akifungua mkutano wa tano wa
Baraza la Mwaka la wadau wa tansia ya nyama nchini jana, Naibu Waziri alisema alisema
pia uzalishaji wa nyama katika machinjio
na sehemu ya kuuzia ni duni na hivyo kusababisha kupoteza soko maalumu la ndani
na kulazimu Serikali kuagiza nyama kutoka nje ya
nchi.
Akielezea kiwango cha ulaji nyama
nchini, Nangoro alisema utafiti umebaini
licha ya Tanzania kuwa na idadi kubwa ya mifugo , ulaji
nyama kwa wananchi wake ni wa
kiwango cha chini.
Kwa mujibu wa naibu waziri,
katika kipindi cha Januari na Februari
mwaka huu , nyama iliyoingizwa nchini ni tani 192 za ng’ombe , 8.2 Kondoo na tani 48.5 za nyama ya nguruwe;
thamani ya tani hizo ni takribani sh bilioni 1.3.
Kwa mujibu wa Naibu Waziri
huyo, kinachosikitishwa zaidi ni ukweli kwamba sehemu kubwa ya nyama hiyo
inatokana na mifugo inayozalishwa hapa nchini.
“ Mifugo hii inasafirishwa kwenda nchi jirani
kwa njia zisizo halali na baadaye kusindikwa na kurudishwa nchini kama nyama
iliyoangizwa toka nje ya nchi na kuuzwa kwa bei kubwa,” alisema.








0 comments:
Post a Comment