Friday, December 21, 2012

TDL Wazindua Kinywaji cha Zanzi

KAMPUNI ya Tanzania Distilleries (TDL) maarufu pia kwa jina la Konyagi ambao ni wazalishaji wa bidhaa za vinywaji vikali na mvinyo hapa nchini, jana walizindua kinywaji kipya kiitwacho Zanzi Cream Liqueur, katika uzinduzi uliofanyika kwenye Hoteli ya Serena, Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa TDL, David Mgwassa, alisema ana uhakika kinywaji hicho kitapendwa na wengi, kwani ni cha Kitanzania na kimezingatia ubora wa kiwango cha Kimataifa katika uzalishaji wake.

Mgwassa aliwataka Watanzania kujivunia kinywaji hicho na kusema TDL ikiwa ni kampuni ya kizalendo itaendelea kuhakikisha inazidi kuitangaza Tanzania kwa kuzalisha bidhaa bora zinazopendwa na wengi ndani na nje ya nchi.

“Kwetu sisi TDL tunajivunia kuzindua rasmi kinywaji cha Zanzi Cream Liqueur kwani kinazalishwa na Watanzania na kimebuniwa na wazalendo wa nchi hii. Huu sasa ni wakati wa kutembea kifua mbele kujivunia kinywaji hiki na naamini kitavutia wengi kutokana na jinsi kilivyotengenezwa na kikiwa na ubora usio na shaka.”

Mgwassa alisema, nia ya kuzalisha kinywaji cha Zanzi Cream Liquer ni baada ya kuona kuna vinywaji vingi vya aina hiyo vikiingizwa nchini kutoka nje, hivyo TDL ikataka kuzalisha bidhaa bora zaidi na ya kipekee hapa duniani.

Naye Meneja Masoko Taifa wa TDL, Joseph Chibehe, alisema kinywaji hicho kitapatikana katika chupa zenye ujazo wa mililita 750 na pakiti zenye ujazo wa mililita 100, huku kikiuzwa kwa bei ambayo watu wengi wataimudu.

0 comments:

Post a Comment