Monday, October 22, 2012

Ogopa Deejayz Kushoot Video ya 'Pete' ya Ben Pol

 
MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Ben Pol, amesema kuwa kutokana na ngoma yake ya ‘Pete’, kufanya vizuri sasa anatarajia kutengeneza video ya ngoma hiyo ambapo kazi hiyo itasimamiwa na timu ya Ogopa Deejays kutoka Nairobi Kenya ambao watatua bongo kupiga kazi......>>>

Alisema kuwa video hiyo gharama yake itakuwa si chini ya milioni 6 kwani ameamua kufanya hivyo ili kutengeneza kazi yenye kiwango na si zile ambazo watu wamekuwa wakizoea kuziona, ambapo anaamini kazi hii itamuwezesha kufanya vizuri zaidi katika muziki wake.
Hata hivyo msanii huyo aliongeza kuwa kufanya kazi na Ogopa ni kufungua njia ya kuvuka mipaka na kuingia Kenya kwani wapo wasanii kibao wa nchini humo anaotaka kufanya nao kazi siku za usoni.

 

0 comments:

Post a Comment