MSANII
wa muziki wa kizazi kipya nchinim Ney wa Mitego, yupo kwenye hatihati ya
kufungiwa na Baraza la Sanaa Tanzania (Basata) baada ya kuachia remix ya wimbo
wake wa Nasema Nao uliojaa matusi na maneno makali dhidi ya wasanii wenzake na
watu mbalimbali.
Kwa
mujibu wa afisa mmoja wa Basata aliyeomba hifadhi ya jina lake kwani si msemaji
rasmi, katika wimbo huo ulioanza kusikika mwishoni mwa wiki iliyopita, Ney wa
Mitego ametumia lugha ya matusi na maneno yasiyo ya kistaarabu, huku akiwataja
kwa majina watu aliowalenga, jambo ambalo ni kinyume na sheria za baraza hilo.
Baada
ya kupata nyepesi hizo kutoka Basata, Showbiz ilimtafuta Ney wa Mitego ambaye
alisema kuwa wimbo huo wa Nasema Nao Remix umevujishwa na watu asiowatambua
bila idhini yake lakini akaeleza hajapokea taarifa yoyote kutoka Basata juu ya
kufungiwa.
GPL
0 comments:
Post a Comment