Thursday, September 13, 2012

Tanzania Live Music Festival kufanyika Leaders



 
Edge Entertainment Co Ltd imeandaa tamasha kubwa la muziki wa dansi linalojulikana kwa jina la Tanzania Live Music Festival litalofanyika kwa muda wa siku mbili kuanzia Septemba 28 na 29, katika viwanja vya Leaders Club kuanzia saa 10:00 alasiri na kuendelea.
Tamasha hili lina lengo la kukuza muziki wa dansi nchini Tanzania, kukusanya fedha kwa ajili ya kukisaidia Chama cha Muziki wa Dansi (chamudata) kiweze kujiendesha kwa ufanisi. Kuchangia mfuko wa sanaa ulio chini ya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA).
Tamasha hili litajumuisha bendi mbalimbali za muziki wa dansi nchini na litakuwa likifanyika kila mwaka, na tunatarajia kwa miaka ijayo kukutanisha bendi mbalimbali nchini na kualika bendi au wanamuziki wakubwa kuja kushiriki toka nje ya Tanzania.
  Katika kufanikisha tamasha tumemchagua Jackline Wolper kuwa Balozi wa tamasha hili kwa mwaka 2012.
 Siku moja kabla ya tamasha 27/9/2012 kutakuwa na mafunzo ya siku moja kwa wanamuziki kuhusu hati miliki yatakayotolewa na COSOTA.
  
Wadhamini wetu ni :TIMES FM RADIO, GLOBAL PUBLISHERS, BUSINESS TIMES, VODACOM TANZANIA

0 comments:

Post a Comment