Wednesday, September 5, 2012

'Izzo Bizness' awakana Mbeya All Stars



Ikiwa ni siku chache baada ya kutoka kwa wimbo ulioshirikisha wasanii kadhaa wakijiita Mbeya All Stars, Rapper Izzo Bizness anayewakilisha mkoa wa mbeya amefunguka kuhusu na kusema hakujua kuhusu hiyo nyimbo wala imetengenezwa wapi na hajahusishwa kwa lolote.
Izzo amesema hajakataa kufanya Mbeya All Stars ila kwa sasa huu mziki ni biashara na kila unachofanya uwe na malengo sio ku copy na kupaste tu.
“Sio sababu flani wamefanya na sisi tufanye, Kigoma All Stars wamefanya kitu kizuri na wamesafiri kwenda Kigoma na Wamefanya show pia wameboresha mambo yao tofauti kupitia udhamini wa hiyo nyimbo, wakati unafanya Project kama hizi lazima ujue lengo lako na sio kufanya kwa kugeza tu”.
Izzo alisema Tayari watu wa Mbeya wanajua anachofanya na anawakilisha vizuri kabisa na hilo ni tosha kabisa kwa mji wake .

0 comments:

Post a Comment